NAMNA YA KUOMBA
- NENO LA MSINGI
YOHANA 16:24
“Hata sasa hamkuomba neno kwa jina langu: OMBENI, NANYI MTAPATA; furaha yenu iwe timilifu”.
Maneno haya aliyasema Yesu Kristo mwenyewe akiwaambia Wanafunzi wake. Tunaona katika maneno haya kwamba, kila mwanafunzi wa Yesu au mtu aliyeokoka, ana haki ya kumwomba Baba yetu aliye mbinguni kwa Jina la Yesu Kristo na akapokea jibu. Yesu hasemi kwamba mtu fulani tu aliyeokoka akiomba, ndiye atakayepata jibu, bali YEYOTE.
MARKO 11:23
“Amin, nawaambia, YEYOTE atakayeuambia mlima huu, ng’oka ukatupwe baharini, wala asione shaka moyoni mwake, ila aamini kwamba hayo asemayo yametukia, yatakuwa yake. Kwa sababu hiyo nawaambia, yoyote myaombayo mkisali, aminini ya kwamba mnayapokea, nayo yatakuwa yenu.”
Maandiko mengi yanadhihirisha jinsi ambavyo kila mtu aliyeokoka alivyo na haki ya kuomba na kupokea jibu na wala siyo mtu fulani pekee. [Angalia mifano katika YOHANA 14:12-14; MATHAYO 7:8-11].
ANGALIA TENA LUKA 11:10; “ Kwa kuwa KILA AOMBAYE HUPOKEA…….”.
Unaona! Kila mtoto wa Mungu, yaani kila mtu aliyeokoka, akiomba, hupokea. Huu ni UHONDO maalum kwa watoto wa Mungu tu. Mtu ambaye hajaokoka, ametenganishwa kabisa na Mungu kutokana na maovu yake. Kutokana na dhambi za mtu ambaye hajaokoka kumfarikisha au kumtenganisha na Mungu, sala zake ni machukizo mbele za Mungu na hazisikilizwi kabisa. [SOMA ISAYA 59:2; MITHALI 28:9; MITHALI 15:29; YOHANA 9:31]. Sala pekee ambayo inasikilizwa na Mungu inapotoka kwa mtu ambaye hajaokoka, ni pale anapotubu dhambi zake na kuwa tayari kuziacha na kuomba damu ya Yesu imsafishe uovu wake; ili aokolewe kutoka katika mauti ya milele [1 YOHANA 1:7-9]. Mtu ambaye hajaokoka, akimpokea Yesu Kristo kuwa Bwana au Mtawala wake na mwokozi wake ndipo anapofanyika MTOTO WA MUNGU na kuanza kufaidi uhondo wa kujibiwa maombi na Baba yetu aliye mbinguni [YOHANA 1:12]. Kabla ya kuokoka, mtu anakuwa ni mtoto wa Ibilisi, na siyo mtoto wa Mungu [YOHANA 8:44]. Kwa sababu hiyo ili uingie katika mpango wa Mungu wa kukupa majibu ya maombi, kwanza ni lazima ukubali kuokolewa na kuwa mtoto wake.
KUTEGEMEA KUOMBEWA NA MWINGINE WAKATI WOTE
Ni huzuni kwamba, wako watoto wa Mungu ambao wanafikiria kwamba wao hawawezi kusikilizwa na Mungu na kujibiwa; mpaka waombewe na mtoto wa Mungu mwingine. Huku ni kukosa ufahamu. Hakuna upendeleo kwa Mungu. Mtoto yeyote katika familia ya Mungu anakubaliwa na Baba aliye Mbinguni. Hakuna mtoto anayekubaliwa na Mungu zaidi anapoomba kuliko mwingine [SOMA MATENDO 10:34-35; WARUMI 2:10-11; KUMB.10:17]. Biblia inasema Mungu hapokei uso wa mwanadamu, yaani hamuoni mtoto wake mmoja kuwa ni bora kuliko wengine kiasi ya kwamba wengine asiwajali [WAGALATIA 2:6]. Eliya alipoomba mvua isinye kwa miaka 31/2; halafu akaomba tena mbingu zikatoa mvua; alikuwa katika hali ya mtoto wa Mungu kama yeyote yule. Alikuwa mwenye tabia moja na sisi, na Mungu hakufanya hayo kwa sababu aliomba Eliya! [YAKOBO 5:17-18].
Watu wengi waliookoka, wanatembea huko na huko katika mikutano wakihitaji kuombewa na watu wengine. Miongoni mwao, wako wanaofikiri sala ya mzungu fulani kutoka Marekani au Uingereza ndiyo ataisikia Mungu zaidi kuliko sala yake. Huku ni kukosa ufahamu. Mungu hapokei uso wa mwanadamu wala hana upendeleo. Kila aaminiye, akiomba hupokea. Ukifanya utafiti, utagundua kwamba, mara nyingi watu ambao wanapokea miujiza wanapoombewa na wengine; ni wale ambao hawajaokoka kabisa, au wale waliookoka lakini wakiwa na muda mfupi sana katika wokovu. Sababu ni kwamba, baada ya mtu kuwa na muda mrefu katika wokovu; unatazamiwa na Mungu kuchukua mwenyewe chakula na kukila bila kungoja kulishwa. Biblia inasema uponyaji ni chakula cha watoto wa Mungu [MATHAYO15:26]. Katika hali ya asili, mtoto anapozaliwa, katika uchanga hulishwa kwa kijiko na mtu mwingine, kwa sababu hawezi kujilisha mwenyewe. Mtoto huyo anapokua, anatazamiwa achukue kijiko na kula mwenyewe. Haitapendeza kumwona mtoto mwenye miaka kumi, akilishwa chakula na mtu mwingine. Vivyo hivyo katika maombi, kila mtu aliyeokoka anatazamiwa kuomba mwenyewe na kuchukua jibu lake. Kwa kukosa maarifa, watu wengi wa Mungu wameangamia [HOSEA 4:6]; na kukosa majibu ya maombi yao. Yafuatayo ni maarifa unayopaswa kuwa nayo ili upate majibu ya maombi yako kila mara.
A: MAMBO MANNE YA KUYAFAHAMU KABLA YA KUMWOMBA MUNGU LOLOTE
1. Mfahamu Vizuri Mungu Baba na Mungu Mwana
Kwa kuwa tunamwomba Mungu Baba kwa jina la Mungu Mwana-Yesu Kristo, ni vema sana kuwafahamu vizuri ili tuwe na hakika ya kujibiwa. Ufahamu ulio nao kuhusu mtu unayekwenda kumwomba hitaji lako, unaweza ukakupa imani ya kupokea kwake au ukakupunguzia imani hata ya kwenda kumweleza hitaji lako. Ukifahamu kwamba mtu fulani ni katili, ufahamu huo unatosha kuondoa ujasiri wa kumwomba lolote. Kwa kukosa kuwafahamu vizuri Mungu Baba na Mungu Mwana, watu wengi waliookoka wamekosa msingi mzuri wa kujibiwa maombi yao. Kinyume na inavyopasa, msingi wao wa kuomba unakuwa ni manung’uniko ambayo huleta maangamizo badala ya mafanikio [SOMA 1 WAKORINTHO 10:10]. Ukiwafahamu vizuri Mungu Baba na Mungu Mwana, ufahamu huo pekee, utakufanya uwe na hakika ya mambo unayotarajia kuyapata; ingawa hayajaonekana bado. Hii ndiyo inayoitwa IMANI ambayo ni msingi muhimu wa kupewa majibu yetu [WAEBRANIA 11:1,6]. Imani ni kuamini jinsi Neno la Mungu linavyoeleza kuhusu Mungu alivyo kwetu. Ukiwafahamu Mungu Baba na Mwana walivyo huwezi kunung’unika, kubabaika na kukata tamaa. Kunung’unika, Kubabaika na Kukata tamaa; ni kinyume kabisa na Imani. Watu wanaonung’unika, kubabaika na kukata tamaa, ni watu wasiomfahamu Mungu alivyo. Usiwe miongoni mwa watu wa jinsi hiyo, ambao hawawezi kupata majibu ya maombi yao.
Inakubidi basi, kuyafahamu yafuatayo na kuyaamini kabla ya kuomba; ili upate Majibu yaMaombi yako:
Mungu Baba hujishughulisha SANA na kila jambo tunalolihitaji, liwe dogo au kubwa. Wakati wote, fahamu kwamba hitaji ulilonalo anapenda kulishughulikia mno. Anataka tu, umtwike YEYE fadhaiko ulilo nalo. [SOMA 1 PETRO 5:6-7].
(b) Ni mapenzi ya Mungu Baba, kukupa haja za moyo wako na kukuona una furaha baada ya kujibiwa maombi [SOMA ZABURI 37:4; YOHANA 16:24].
(c) Mungu Baba anawahurumia watu waliookolewa kama vile Baba awahurumiavyo watoto wake [SOMA ZABURI 103:13]. Linalofurahisha zaidi ni kwamba, Mungu Baba; ni Baba mwenye uwezo wote, tofauti na baba wa duniani ambao wanaweza kuwa na huruma kwa watoto wao, lakini wakakosa uwezo wa kuwasaidia; wakabaki kusema “POLE”, bali huruma ya Mungu huambatana na UWEZO wa kutupa mahitaji yetu; hata yakiwa mazito kiasi gani. [ANGALIA MFANO LUKA 7:13-15].
(d) Mungu kamwe hawasahau, hawaachi, hawapungukii wala hawatupi watoto wake yaani watu waliookoka. Unapokuja mbele za Mungu ukiwa unajiona umeachwa, umesahauliwa au umetupwa; basi ujue unampa nafasi shetani ya kukuangamiza kwa kukosa maarifa ya Neno la Mungu. Tunaweza tu kumshinda shetani kwa “Imeandikwa” yaani kwa Neno la Mungu, kama Yesu alivyomshinda alivyokuwa anajaribiwa na Ibilisi nyikani. Mbinu kubwa ya Ibilisi anayotumia kumshinda mtu aliyeokoka, ni kumfanya akiri tofauti na “Imeandikwa”. Unachotakiwa kufahamu kuanzia leo ni kwamba, Imeandikwa kuwa Mungu hawezi kumsahau, kumuacha au kumtupa mtoto wake, yaani mtu aliyeokoka. Wewe unaweza kumwacha, lakini yeye hawezi kukuacha katika mahitaji unapokaa ndani yake. [SOMA KWA MAKINI ZABURI 94:14; KUMBUKUMBU 31:8; ISAYA 49:14-16; ZABURI 37:25; 1 SAMWELI 12:21-22; 1 WAFALME 6:13; ZABURI 37:28].
(e) Ikiwa Mungu Baba alimtoa mwanawe wa pekee Yesu Kristo ili afe kwa ajili ya dhambi zetu, je hatazidi sana kutupa mambo mengine tunayoyahitaji, ambayo thamani yake siyo kubwa kama thamani ya mwanae wa pekee? [SOMA WARUMI 8:32].
(f) Yesu Kristo ni mzaliwa wa kwanza katika uzao wa Adamu wa pili yaani uzao wa watu waliookoka. Ni kusema kwamba, Yeye ni NDUGU yetu. Yeye ni KAKA YETU wa kwanza kuzaliwa. [SOMA WARUMI 8:29; WAEBRANIA 2:11]. Tafakari jinsi alivyo ndugu wa kwanza kuzaliwa katika familia, hasa anapokuwa wa kiume. Mahitaji yote ya wadogo zake, huyabeba yeye. Ni kaka yupi mwenye uwezo wote wa kuwasaidia wadogo zake, ambaye atawaacha ndugu zake bila msaada? Ikiwa kaka wa duniani wasiokuwa na uwezo wote, wanajitahidi kuwasaidia wadogo zao; ni zaidi sana kwa kaka yetu Yesu Kristo mwenye upendo wote na uwezo wote mbinguni na duniani. Anahusika MNO NA KILA HITAJI walilo nalo wadogo zake. Ndiyo maana anamwita mdogo wake yeyote mwenye kusumbuka na kulemewa na mzigo wowote, aende kwake ampumzishe. [MATHAYO 11:28]. Yesu anataka tumtwike mizigo yetu yote na masumbufu yetu yote, kama jinsi ambavyo Baba anavyotaka tumtwike fadhaa zetu zote!
2. Fahamu jinsi ulivyo wa thamani mbele za Mungu
(a) Wewe ni TAJI YA UZURI katika mkono wa BWANA [ISAYA 62:3]. Jiulize mwenyewe, taji ya uzuri utakubali ichafuliwe na tope au ichanwe? Utaitunza na kuiangalia namna gani?
Wewe ni KILEMBA CHA KIFALME mkononi mwa Mungu wako [ISAYA 62:3]. Kilemba cha kifalme ni kitu cha thamani mno. Kinazidi thamani yake kinapokuwa ni kilemba cha kifalme cha Mungu. Wewe ni kilemba cha Kifalme cha Mungu. Wewe ni wa thamani mno machoni pa Mungu. Jiulize mwenyewe, Mungu ataacha kukitunza kilemba chake cha kifalme?
(b) Anayekugusa wewe na kukutesa, kukuonea, au kukukosesha furaha, anakuwa anaigusa mboni ya jicho la Mungu [ZEKARIA 2:8]. Ikiwa wewe huwezi kukubali kuweka kidole kwenye mboni ya jicho la Mungu. Atafukuzwa kwa utisho mkuu.
(c) Katika mpango wa Mungu, Yesu alikuokoa wewe na kukutoa mahali palipokuwa pakame na jangwa tupu lisilokuwa na matumaini; na kukulaza kwenye majani mabichi. Hataki tena upungukiwe na kitu [ZABURI 23:1-2]. Zaidi ya hayo, kwa kuwa wewe ni wa thamani mno kwake, anakuzunguka na kukulinda kwa uwezo wake wote. Mpango wake, ni kukutunza na kukuhifadhi kama mboni ya jicho [SOMA KUMBUKUMBU 32:10]. Jiulize mwenyewe, Je, unaitunza namna gani mboni ya jicho lako? Kipande kidogo tu cha mchanga kikiingia jichoni, utahangaika mno mpaka kitolewe. Utairuhusu miiba ikaribie kwenye mboni ya jicho lako? Mboni ya jicho ikiingiwa na vumbi kidogo tu, jicho lote hujaa machozi na mwili wote kuhuzunika. Furaha huja tu pale vumbi linapotoka. Ndivyo alivyo Yesu pia unaposumbuliwa wewe mboni ya jicho lake, yeye pia hulia machozi pamoja nawe na kuhakikisha kila kinachokusumbua kinatoweka [YOHANA 11:33-36, 43-44].
(e) Wewe ni KITO AU JIWE LA THAMANI LINALOMETAMETA katika nchi ya Mungu[ZEKARIA 9:16]. Jiwe la thamani linaangaliwaje? Hazina inashughulikiwaje?
(f) Wewe ni HAZINA YA MUNGU [SOMA MALAKI 3:16]. Hazina inalindwaje? Hazina inaangaliwaje? Hazina inatunzwaje? Hazina inashughulikiwaje?
(g) Wewe ni MALI ILIYONUNULIWA KWA THAMANI KUBWA. Ulinunuliwa kwa damu ya YESU ya thamani. [SOMA 1 WAKORINTHO 7:23; 1 WAKORINTHO 6:20]. Jiulize mwenyewe! Mali uliyoinunua kwa thamani kubwa, unailinda na kuitunza namna gani? Mwanadamu anaweza kuwa mzembe, asijue sana kutunza mali; lakini Mungu asiye mzembe kamwe, hakika atakutunza. Wewe ni wa thamani mno kwake!
Wewe ni BIBI-HARUSI, MKE WA MWANA-KONDOO yaani MKE WA YESU [SOMA UFUNUO 21:9]. Biblia inasema, “Kama Bwana-Arusi amfurahiavyo Bibi-Arusi, ndivyo Mungu anavyokufurahia wewe.” [SOMA ISAYA 62:5]. Ikiwa Yesu anakufurahia hivi kama Bibi-Arusi wake, je atakuacha kabisa na asikujali au asikupe mahitaji yake? Dalili ya kumfurahia Bibi-Arusi, ni kuhusika sana na mahitaji yake. Bibi-Arusi anapoomba lolote kwa Bwana-Arusi, mara moja Bwana-Arusi hufanya jitihada yote ili ampe na kumfurahisha. Mabwana-Arusi wa duniani hawana uwezo wote, hivyo hukwama katika kuwatekelezea mahitaji yao yote Mabibi-Arusi wao; lakini Bwana-Arusi Yesu Kristo mwenye uwezo wote, kamwe hashindwi. Lolote unalolihitaji kwake, atakupa ili akufurahishe. Mungu ni MUME WAKO! [SOMA YEREMIA 3:14]. Huu ni ukweli wa ajabu! Ikiwa mumeo ni Rais wa Nchi, utakuwa na hakika ya kutunzwa, kuangaliwa na kupewa mahitaji yako! Hata hivyo Rais wa Nchi ana mpaka. Hawezi kukupa mahitaji yako yote. Sasa tafakari ukweli huu kwamba Mungu aliye muumba wa mbingu na nchi ni mumeo! Una haki ya kuringa, kuwa na mume wa namna hii mwenye uwezo wote. Je atashindwa kukupa nini? Ana uwezo wa kutuma watumishi wake malaika, wakuletee chochote ukitakacho.
3. Fahamu kwamba hakuna gumu lisilowezekana kwa Mungu:
Usiupime kamwe uwezo wa Mungu kwa kuulinganisha na uwezo wa mwanadamu. Kufanya hivyo, ni kama kuulinganisha uwezo wa kuangaza kwa JUA na KOROBOI! Kulinganisha kiasi cha uwezo wa Mungu wa kufanya jambo na uwezo wa mwanadamu, ni kama kulinganisha kiasi cha maji kinachotosha kuijaza bahari, na kile kinachotosha kujaza kikombe. Kwake Mungu, hakuna neno ‘HAIWEZEKANI’. Hili ni neno la kibinadamu tu! Mungu anasema ingawa jambo linaweza kuwa haliwezekani mbele za wanadamu na kuwa gumu mno lakini siyo mbele za Mungu. Angalia maandiko.
ZEKARIA 8:6
“Bwana wa majeshi asema hivi, Ingawa hili ni neno lililo gumu mbele ya macho ya mabaki ya watu hawa siku hizo, je! liwe neno gumu mbele ya macho yangu? asema BWANA wa majeshi.
“SOMA PIA YEREMIA 32:17, 27; AYUBU 42:2; MATHAYO 19:26; LUKA 1:37”.
4. Fahamu kwamba magonjwa na umasikini siyo mapenzi ya Mungu kwako:
Magonjwa na umasikini au kutofanikiwa, ni sehemu ya LAANA juu ya mtu asiyetaka kuisikiliza sauti ya BWANA Mungu na kufanya maagizo yake [KUMBUKUMBU 28:15-28]. Yesu alifanyika laana kwa ajili yetu kwa kupigiliwa msalabani ili baraka zitufikie [WAGALATIA 3:13-14]. Kwa kupigwa kwake Yesu na hatimaye kusulubishwa msalabani, alitukomboa kutoka katika:-
(a) Dhambi [MATHAYO 26:28; 1 PETRO 2:24].
(b) Magonjwa na udhaifu wote [MATHAYO 8:14-17; ISAYA 53:4-5;
1 PETRO 2:24].
(c) Umasikini [ 2 WAKORINTHO 8:9].
Magonjwa na udhaifu wote, umasikini na dhambi; zote ni kazi za Ibilisi ambazo zilivunjwa na Mwana wa Mungu [1YOHANA 3:8]. Watu tuliookolewa, hatuko tena chini ya laana. Hivyo kama unavyozikataa na kuzipinga dhambi,vivyo hivyo inakupasa kuyakataa na KUYAPINGA MAGONJWA na Udhaifu wote, na kuukataa umasikini. Hivyo usiseme “Labda ni mapenzi ya Mungu niugue” au “Huenda anataka kunifundisha kwa ugonjwa”. Ni mapenzi ya Mungu UWE MZIMA WA AFYA – Yeye anaitwa YEHOVA-RAPHA AU “BWANA NIKUPONYAYE” [SOMA KUTOKA 15:26; YEREMIA 30:17; YEREMIA 33:6; ZABURI 103:3; YOHANA 10:10; 3 YOHANA 1:2].
Mungu ana njia nyingi za kukufundisha. Hakufundishi kwa kumruhusu shetani akuletee magonjwa! Ukisema ni mapenzi ya Mungu uugue, basi ujue unazidi kumpa nafasi shetani akutese zaidi. Mapenzi ya Mungu, ni Neno la Mungu. Shetani akijua kwamba hulijui neno lililoandikwa, atakutesa! Usimpe nafasi Ibilisi kwa kuzungumza yaliyo kinyume na Neno la Mungu. Mara zote, yapinge magonjwa ukijua kwa kufanya hivyo unampinga shetani; naye atakimbia. Shetani ndiye mleta magonjwa yote. Shetani ndiye aliyeleta magonjwa juu ya Ayubu na kutofanikiwa kote. Ayubu hakujua akasema ni Mungu! Usiwe kama Ayubu. Mjue mbaya wako Shetani! [Angalia WAEFESO 4:27; YAKOBO 4:7; AYUBU 1:12-16; AYUBU 2:2,7]. Hivyo kumbuka kwamba usitumie “Ikiwa ni mapenzi yako” katika kuomba juu ya ugonjwa. Tunatumia maneno haya pale tu tusipokuwa na uhakika wa jambo. Uhakika juu ya ugonjwa uko tayari katika Neno. Ni mapenzi ya Mungu uwe mzima.
B. UKIYAJUA HAYA MWELEZE MUNGU HAJA ZAKO KWA MAOMBI:
Bila mashaka ya kupokea majibu, wewe kama Bibi Arusi mwendee Mume wako Mungu, na kumwelezea unalolihitaji. Maombi ni mazungumzo na Mungu. Zungumza naye kama jinsi ambavyo unavyoweza kuzungumza na mumeo, Rafiki yako, Baba yako au Kaka yako. Usimwendee huku ukinung’unika, ukilia na kubabaika; kiasi ya kwamba hata unalolihitaji halifahamiki! Usiseme yeye anajua yote, hivyo huna haja ya kumweleza kitu. Hivyo siyo sawa na Neno la Mungu. Utampa nafasi Shetani kukupiga kwa kusema hivyo, maana hulijui Neno la Mungu. Mpango wa Mungu wa sisi kupokea, ni KUMWOMBA tukimweleza mambo yote tunayoyahitaji [ISAYA 43:26; YOHANA 16:23-24; YOHANA 15:7]. Kumbuka Neno linavyosema “Kila aombaye hupokea.” Ni kwa sababu hii huna haja ya kutaka watakatifu fulani waliokufa wakuombee! Siyo Bikira Maria, Petro, Paulo au yeyote. Yesu mwenyewe kwa pendo lake, ndiye pia Mwombezi wetu kwa Baba. Hakuna mwingine mbinguni! [1 YOHANA 2:1]. Kwa Imani tu, zungumza na Mungu bila kutumia vitu vingine na kuviweka kati yako na Mungu kwa mfano Rozari, Maji ya Baraka n.k. Aliye kati yetu na Mungu anapaswa kuwa YESU tu! Watu wengine husema kwamba hawajui kuomba kwa kutokujua maana ya maombi. Kama ulivyotangulia kufahamu, maombi ni mazungumzo. Mke anazungumzaje na Mumewe? Ebu angalia mfano huu:- “Mume wangu, naomba fedha nikanunue mafuta ya kujipaka. Ngozi imechubuka sana kutokana na jua kali. Nimeona mafuta mazuri yanauzwa kwa shilingi mia moja.”
Kwa jinsi hii hii, ndivyo tunavyozungumza na Mungu. Ni jinsi ile ile mtoto anavyomwomba Baba yake kalamu ya kuandikia shuleni.
C. TUMIA MAMLAKA ULIYO NAYO JUU YA SHETANI KATIKA MAGONJWA NA ONDOA VIZUIZI VYAKE VYOTE VYA MAJIBU.
Hapo mwanzo, Adamu alikuwa na mfano wa Mungu katika utakatifu mpaka pale alipotenda dhambi kwa kutumia vibaya hiari yake ya kuchagua jambo la kufanya. Akachagua kuliasi Neno la Mungu, tendo ambalo ndilo linaloitwa dhambi. Kabla Adamu hajafanya dhambi, alikuwa ni MTAWALA. Chochote katika nchi kilipaswa kumtii Adamu. Hii ni pamoja na Shetani. Adamu alipofanya dhambi na kukubali Neno la Shetani, alipoteza mamlaka ya utawala aliyokuwa nayo na akayachukua Shetani. [MWANZO 1:26-27]. Alipokuja Yesu na kututoa katika utumwa wa dhambi, na kuzivunja kazi za Ibilisi aliyetutumikisha wote tuliozaliwa kutokana na Adamu; alifanya jambo jingine zuri. Aliturudishia mamlaka aliyotunyang’anya Shetani. Ndiyo maana Yesu alisema “Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani baada ya kufufuka [MATHAYO 28:18]. Sasa mamlaka hii aliyoichukua Yesu ni ile aliyokuwa ametunyang’anya Shetani. Kwa kumshinda Shetani na kazi zake zote, Yesu alimnyang’anya mamlaka Shetani na kutupa mamlaka hiyo ambayo pia inaitwa “AMRI”. Kwa mamlaka hii au “AMRI” aliyoturudishia kila mtu aliyeokoka ana uwezo wa kumkanyanga nyoka yuleyule aliyetukanyaga mwanzo. Nguvu zote za Shetani, hazina uwezo juu ya mtu aliyeokoka.
LUKA 10:18-19
“Akawaambia, Nilimwona Shetani, akianguka kutoka mbinguni kama umeme. Tazama nimewapa AMRI ya kukanyanga nyoka na nge, na NGUVU ZOTE ZA YULE ADUI (SHETANI), wala hakuna kitu kitakachowadhuru.” Nguvu zozote za Shetani hata kama zingekuja kwa vitisho kama umeme, ziko chini ya “AMRI” au “MAMLAKA” ya mtu aliyeokoka. Unapolitumia Jina la Yesu kwa Mamlaka au Amri juu ya pepo wanaosababisha tatizo ulilo nalo, pepo hao watakutii na kuondoka [SOMA LUKA 10:17]. Magonjwa mengi husababishwa na pepo wa udhaifu [SOMA LUKA 13:11; MATHAYO 12:22;MARKO 9:17, 25; LUKA 11:14]. Unapokuwa umeelemewa na ugonjwa wowote iwe ni homa au ugonjwa wowote, au unapokuwa unaomba kwa ajili ya ugonjwa alio nao mwenzio; haitoshi tu kumwomba Mungu auponye ugonjwa huo, ila inakubidi pia UTUMIE MAMLAKA ULIYO NAYO JUU YA SHETANI NA KUUKEMEA UGONJWA HUO NA KUUAMURU KWA AMRI KWAMBA UHAME. [Angalia mfano katika [LUKA 4:38-39].
MFANO WA MAMLAKA KATIKA ULIMWENGU HUU:
Waangalie askari wa Usalama Barabarani au askari wa trafiki. Hata kama umbo la askari ni dogo namna gani, kwa kutumia mamlaka aliyopewa na Serikali, anaponyosha mkono mtupu usio na chochote, gari kubwa lenye tela nyuma na linaloendeshwa na mtu mwenye umbo kubwa husimama pale pale. Vivyo hivyo kwa mtu aliyeokoka. Hata kama ukiwa na umbo dogo namna gani au umeokoka leo tu au jana, unapoamuru pepo wa udhaifu au kazi yoyote ya Shetani ikuachie bila mashaka yoyote, kazi hiyo ya Shetani itahama. Mamlaka uliyopewa na Yesu ni kubwa mno. Unapolitumia Jina la Yesu, ni kwamba unamwakilisha Yesu mwenyewe kama jinsi ambavyo askari wa Usalama Barabarani anavyoiwakilisha Serikali. Askari wa Usalama Barabarani anaponyosha mkono kuamuru gari kusimama, huwa hana mashaka ndani yake kwamba labda gari hilo litaendelea kwenda. Ni lazima dreva huyo atatii na kulisimamisha gari. Vivyo hivyo kwako, inakupasa kutoa mashaka unapomkemea Shetani kuhama; naye lazima atakutii [LUKA 10:17]. Unapokuwa pia ukiomba, kumbuka kukemea namna zozote za vizuizi vya Shetani juu ya majibu ya maombi yako. Shetani hutumia wakuu wake wa giza walio chini yake KUCHELEWESHA MAJIBU ya Maombi ya Watakatifu [ANGALIA MFANO KATIKA DANIEL 10:12-13].
D. BAADA YA MAOMBI, AMINI KWAMBA UMEPOKEA MAJIBU NA USIKUBALI KUTEGWA NA SHETANI KWA MANENO
Biblia inasema katika MARKO 11:24, “Kwa sababu hiyo nawaambia, yoyote myaombayo mkisali, AMININI YA KWAMBA MNAYAPOKEA nayo yatakuwa yenu”. Hali unayokuwa nayo BAADA ya maombi ni muhimu sana kama unataka kuona muujiza wako au jibu la maombi yako. Kamwe usikubali kuongozwa na milango mitano ya fahamu baada ya maombi. Usiongozwe na KUONA AU HISIA! Ya kwamba unajisikiaje au unajionaje baada ya maombi, hayo siyo muhimu. Hatuenendi kwa kuona bali kwa imani [SOMA 2 WAKORINTHO 5:7] Wakati mmoja, Yesu aliulaani mtini usiokuwa na matunda. Wanafunzi wakasikia alivyotoa amri juu ya mti ule, lakini halikuonekana badiliko lolote la kuonekana machoni wakati huo huo. Kesho yake asubuhi wanafunzi wale ndipo wakashangaa kuona mtini ule umenyauka kutoka shinani. Wakamwambia Yesu kwamba mtini ule umenyauka (BAADA YA KUONA!) . Yesu akawajibu “MWAMININI MUNGU”. [SOMA MARKO 11:12-14, 20-21]. Maana yake nini? Palepale Yesu alipotoa amri, mti ule ulinyauka kutoka kwenye MIZIZI! Macho hayaoni mizizi ya mti maana iko chini ya udongo. Kesho yake, kunyauka huko kulikwisha fika kwenye shina na kwenye matawi mahali ambapo macho yanapoona. Jina la Yesu katika amri linashughulikia MZIZI WA TATIZO ili kukuweka huru kabisa. Macho yanachukua muda kuona wakati mwingine. Macho hungoja kuona shina na matawi. Kungoja kuona kwa macho siyo Imani na huua kabisa matokeo ya maombi. Kumbuka baada ya maombi kwamba hata kama majani kwenye matawi yanaendelea kuwa kijani kibichi, yatakauka tu kwa kuwa mizizi ya mti imenyauka. Usikiangalie kichwa au tumbo linaloendelea kuuma baada ya maombi. Mzizi umenyauka! Tumbo lazima litaacha kuuma.
Unalotakiwa kufanya baada ya maombi ni KUKIRI USHINDI kwa maneno ya kinywa chako. Mungu aliumba mbingu na nchi kwa Neno. Na iwe hivi ikawa hivyo. Neno la Mungu lina uwezo wa kuumba. Kwa jinsi hiyo hiyo, mtoto wa Mungu ana uwezo wa kuumba kwa maneno yake. Kwa maneno yako, utashiba mema au mabaya [SOMA KWA MAKINI MITHALI 18:20-21]. Baada ya maombi, Shetani hungoja kukutega kwa maneno ya kinywa chako. Maneno yako yasiyokiri ushindi humfanya mwindaji au mtega mitego Shetani kukushinda tena na kuendelea kukuonea. Kujiponya katika mtego wake, ni kukiri ushindi.
MITHALI 6:2,5:
“Basi umetegwa kwa maneno ya kinywa chako, umekamatwa kwa maneno ya kinywa chako. Ujiponye kama paa na mkono wa mwindaji, na kama ndege katika mkono wa mtega mitego”.
Jambo muhimu la kukumbuka ni kwamba kukiri ushindi kwa maneno ya kinywa chako siyo kibali cha kusema uongo. Ikiwa ulikuwa unaomba nyumba na hujaipata baada ya maombi, usiseme “Nimekwisha pata nyumba nzuri sana iko Sinza, Dar es Salaam.” Huo ni uongo ambao unampa nafasi zaidi Shetani ya kukukosesha muujiza. Kama bado kichwa kinauma na homa inaendelea baada ya maombi unapoulizwa usiseme “Kuuma kichwa na homa, vyote vilikwisha toweka zamani”. Kama bado ni kipofu baada ya maombi usiseme “Ninaona sasa bila matatizo.” Huo wote ni uongo. Biblia inatukataza kumtetea Mungu kwa kusema uongo kwa ajili yake. [AYUBU 13:7-8].
Kukiri ushindi kwa maneno yako baada ya maombi, ni kukiri maneno ya Mungu ya ushindi bila kujali mazingira uliyo nayo au hali uliyo nayo baada ya maombi. Kwa mfano, “ Kwa kupigwa kwake,mimi niliponywa”[1 PETRO 2:24]; “Aliyachukua masikitiko yangu na huzuni zangu. Kwa kupigwa kwake mimi nilipona” [ISAYA 53:4-5]; “Siku za njaa nitashiba, sitaaibika wakati wa ubaya.” [ZABURI 36:19]; “Wamtafutao BWANA hawatahitaji KITU CHOCHOTE kilicho chema”. [ZABURI 34:10]; “Yesu amekuja ili niwe na uzima, tena niwe nao tele”. Mungu anapenda nifanikiwe katika mambo yote. Kwa maneno haya, tatizo langu limekwisha.”[YOHANA 10:10; 3 YOHANA 1:2] n.k.
Usiseme maneno kama yafuatayo, ukatengwa na kukamatwa na Shetani na kushindwa: “Labda nitapona”. “Mungu akipenda nipone, nitapona.” “Hali yangu imezidi kuwa mbaya baada ya maombi, nafikiri ugonjwa huu utaniua.” – Ukisema hivi, utakufa kweli, utapata matunda ya kinywa chako! Baada ya maombi, kiri maneno ya Mungu ya Ushindi bila kuangalia maumivu yanayoendelea au mazingira yanayokukabili wakati huo.
VIZUIZI KUMI VINAVYOFANYA MAMLAKA YAKO ISITENDE KAZI KUBWA
NA KUWEZA KUPATA MAJIBU YA MAOMBI KWA KIWANGO CHA JUU
Yesu alisema kwamba yeye amwaminiye, atazifanya kazi alizozifanya yeye na hata kubwa zaidi kuliko alizozifanya Yesu. [SOMA YOHANA 14:12]. Lakini leo utaona kwamba watu wengi wanaomwamini Yesu, wanasumbuliwa na kazi ndogo tu za Shetani na mamlaka yao inashindwa kutenda kazi. Viko vizuizi vinavyosababisha mtu asione miujiza mikubwa inayotokana na maombi na mamlaka yake juu ya Shetani:-
(1) Kutaka miujiza tu na ukawa hutaki kumfuata Yesu katika mambo yote
[MATHAYO 6:33; YOHANA 6:24-27; ZABURI 91:14-16].
(2) Yesu alikuwa chini ya amri ya Baba wakati wote. Baba alivyomwamuru ndivyo alivyofanya. [YOHANA 14:31]. Hii ndiyo iliyokuwa siri kubwa ya Yeye kutenda kazi kubwa na kuwa na mamlaka yote juu ya Shetani. Leo watu wengi waliookoka hawataki kuwa chini ya amri ya Baba yaani kufuata amri zote katika Neno la Mungu. Wanaongeza na kupunguza katika Neno la Mungu na kuchagua yale yaliyo rahisi kwao kuyafanya. Kufanya hivyo ni machukizo na kutafuta kupigwa na Shetani. [KUMBUKUMBU 4:2; 12:32; MITHALI 30:5-6; UFUNUO 22:18-19]. Kufanya yote aliyoamriwa, ndiyo ilikuwa siri ya Yoshua kufanya kazi kubwa na kuwa na mamlaka kuu juu ya Shetani. Alipoamuru Jua kusimama, lilitii. Siri ya ushindi huo, ni Yoshua kufanya YOTE aliyoamriwa na Mungu kupitia kwa Musa. [YOSHUA 11:15]. Ukitaka kuona mamlaka yako inatenda kazi kubwa, mtii aliyekupa mamlaka na kuyafanya yote anayokuamuru. Usiseme kufanya hili na hili siyo lazima. Usiseme kubatizwa katika maji tele baada ya kuamini siyo lazima; usiseme kutoa fungu la kumi katika mapato yako yote siyo lazima. Usiseme kuvaa mavazi ya kidunia na kufanana na mataifa siyo tatizo. Ukichagua ya kufanya, mamlaka yako inakuwa dhaifu sana. Hakikisha siku zote maisha yako yote yanakuwa sawa na HESABU 23:26. Siku zote wafukuze watenda mabaya wanaokushawishi kuacha kuyatenda maagizo yote ya Mungu [SOMA ZABURI 119:115].
(3) Kutafuta kuwapendeza wanadamu badala ya Mungu. Yesu siku zote
alihakikisha anafanya kila njia kumpendeza Mungu siku zote. Hii ndiyo siri nyingine ya nguvu yake ya maombi. [SOMA YOHANA 8:29]. Tatizo kubwa kwa watu wengi waliookoka, wanatafuta kuwapendeza wanadamu na kuonekana wazuri kwao, badala ya kutafuta kumpendeza Mungu. Mashujaa wote waliokuwa na uwezo mkubwa katika maombi yao, walikuwa wanatafuta kumpendeza Mungu kabla ya yeyote. Hii ndiyo iliyokuwa siri ya ushindi kwa Daudi na kuwa na uwezo wa kumpiga Goliathi kwa jiwe MOJA tu lililokuwa kwenye kombeo. [SOMA ZABURI 73:25].
(4) Kuigeukia miungu mingine. Kazi yako, biashara yako, mchumba wako, ndugu
zako, wazazi wako, masomo yako au vitu vyako vinaweza kuwa ni miungu yako ikiwa vinakufanya ukose nafasi ya kumwabudu Mungu, kufanya kazi yake, na kuwa na usharika naye. Jambo hili husababisha uso wa Mungu ufichwe kwako, na usione majibu ya maombi. [SOMA KUMBUKUMBU 31:18].
(5) Ikiwa viungo vyako vya mwili vinatumika kutenda dhambi, Mungu anapoviangalia, anaviona vimejaa damu na uchafu. Vidole vinavyoshika sigara, mikono inayotumika kushika bia, midomo inayotumika kusema uongo na kusengenya, miguu na viuno vinavyotumika kucheza Disco na Ngoma, viungo vyako vya siri vinavyotumika kufanya uasherati na uzinzi, macho yako yanayotumika kuangalia sinema na video za kidunia, masikio yako yanayojistarehesha kwa kusikia miziki ya kidunia katika radio n.k. Kila kiungo kinachotumika kutenda dhambi, mbele za Mungu kinakuwa kimejaa damu na uchafu na kinafanya uso wa Mungu ufichwe kwako na usione majibu ya maombi kwa kiwango cha juu [SOMA ISAYA 1:15; EZEKIELI 39:24; ISAYA 59:2-3].
(6) Kutokuwa tayari kujifunza Neno la Mungu na kulitenda. Wako watu wengi waliookoka ambao baada ya kuokoka, hawaoni umuhimu wa kutafuta mafundisho kwa bidii bali wanazunguka huko na huko kutafuta mikutano ya Injili tu. Baada ya kuokolewa, hupaswi kutafuta Injili ya kukuokoa tena! Inakupasa kutafuta mafundisho au maarifa. Ukichukia maarifa, majibu ya maombi yako yanakuwa hafifu [SOMA MITHALI 1:28]. Yesu alinena kama Baba ALIVYOMFUNDISHA [ANGALIA YOHANA 8:29]. Ikiwa Yesu alikubali kufundishwa, ni zaidi sana sisi. Hiyo ndiyo iliyokuwa siri ya ushindi wake na kwa unyenyekevu anatuonyesha siri hiyo. Unapokubali kutafuta mafundisho ya KWELI hata yakiwa magumu namna gani, ujue kweli hiyo ndiyo itakayokuweka huru wakati wote. Maneno ya Mungu yakiwa kwa wingi ndani yako, majibu ya maombi yako yatakuwa dhahiri. [SOMA YOHANA 8:31; YOHANA 15:7]. Kumbuka pia kwamba kulijua Neno la Mungu bila kulitenda ni kuwa sawa na Shetani. Yeye analijua Neno la Mungu lakini halitendi. Ili uwe tofauti na yeye na kumshinda kwa mamlaka, sikiliza lolote katika neno na kulitenda au siyo, utalia na usisikilizwe na BWANA (SOMA KUMBUKUMBU 1:43, 45).
(7) Mashaka kabla au baada ya maombi, huzuia kabisa majibu ya maombi. Bila mashaka au kusitasita, mwendee Mungu ukijua hakika atafanya. [SOMA YAKOBO 1:6-7; WAEBRANIA 10:38; MARKO 11:23].
(8) Makusudi yako ya maombi ni lazima yawe ya kupata na kulitumia jibu kwa
utukufu wa Mungu na siyo kwa tamaa tu! [YAKOBO 4:3; 1 WAKORINTHO 10:31].
(9) Kumpiga mkeo, kutompa heshima na kumuonea tu kwa kuwa ni chombo
kisicho na nguvu; jambo hili husababisha pia maombi yako kuzuiliwa na kutopata majibu[SOMA 1 PETRO 3:7].
(10) Kutohubiri Injili kwa watu ambao hawajaokoka pia husababisha mamlaka yako
kupungua na majibu yako ya maombi kuwa mbali. Watu ambao hawajaokoka ni maskini wanaohitaji habari njema. Yesu aliwahubiria maskini hawa habari njema. Ukiziba masikio usisikie kilio chao cha kutaka habari njema, na kuwaacha waende Jehanum, wewe pia maombi yako hayatasikiwa [SOMA MITHALI 21:13]
Ukikaa katika mafundisho haya, utajua kwamba Mungu wetu yuko karibu mno na anajibu kila tumwitapo [SOMA KUMBUKUMBU LA TORATI 4:7]. - See more at: http://www.gospelkitaa.co.tz/2014/06/somo-jinsi-ya-kuomba-mwenyewe-na-kupata.html#sthash.gHh3IFml.dpuf

Katika mwongozo huu tunaona jinsi maombi yanavyotusaidia kujenga uhusiano wenye nguvu zaidi pamoja na maisha ya Kikristo yenye nguvu.
1. Kuzungumza Na Mungu
Je, tunawezaje kuwa na uhakika kwamba Mungu anatusikia tunapoomba?
"Ndipo mtaniita mimi na kwenda KUNIOMBA, nami NITA SIKILIZA. Nanyi mtanitafuta na kuniona, mtakaponitafuta kwa moyo wenu wote." - Yeremia 29:12,13.
Je, ni uthibitisho gani aliotoa Yesu kuonyesha kwamba atasikia na kujibu maombi yetu?
"Basi nawaambia, Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi mtaona; bisheni, na mlango utafunguliwa kwenu." - Luka 11:9.
Maombi ni maongezi ya pande mbili. Hii ndiyo maana Yesu anaahidi anasema:

Kwa jinsi gani inawezekana kwetu kuketi na kuwa na maongezi mazuri wakati wa chakula cha jioni pamoja na Kristo? Kwanza, kwa kumwambia kila kitu tulicho nacho moyoni mwetu kwa njia ya maombi. Pili, kwa kusikiliza kwa makini. Tunapotafakari wakati wa maombi, Mungu anaweza kuongea nasi moja kwa moja. Na tunapolisoma Neno la Mungu kwa roho ya ibada, Mungu ataweza kuongea nasi kupitia katika kurasa zake.
Maombi yanaweza kuwa njia ya maisha kwa Mkristo.
"OMBENI BILA KUKOMA; shukuruni kwa kila jambo, maana hayo ndiyo mapenzi ya Mungu kwenu katika Kristo Yesu." - 1 Wathesalonike 5:16-18.
Je! sisi tunawezaje "kuomba bila kukoma?" Je, yatupasa kupiga magoti wakati wote au kurudia-rudia kusema maneno ya kumsifu au kutoa dua? La, hasha. Lakini tunapaswa kuishi karibu sana na Yesu kiasi cha kujisikia huru kusema naye wakati wo wote, na mahali po pote.
"Tukiwa katika makundi ya watu mitaani, katika shughuli ya kibiashara, tunaweza kutoa dua yetu kwa Mungu na kumsihi atupe uongozi wake… Daima tungeacha wazi mlango wa moyo wetu na kuuacha mwaliko wetu ukipanda juu ili Yesu aweze kuja moyoni mwetu na kukaa humo kama mgeni wetu wa mbinguni." - Steps to Christ, uk. 99.
Mojawapo ya njia bora sana ili kujenga uhusiano huo wa karibu sana ni kujifunza kutafakari wakati tunapoomba.
"Kutafakari kwangu na kumpendeze yeye, mimi ninapomfurahia BWANA." -Zaburi 104:34.
Unapoomba usiharakishe tu kupitia orodha ya mambo unayotaka. Ngojea. Sikiliza. Kutafakari kidogo ukiwa katika maombi kunaweza kuuboresha sana uhusiano wako na Mungu.
"Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi." - Yakobo 4:8.
Kadri sisi tunavyozidi kumkaribia sana Yesu ndivyo kadri tunavyoweza kuonja kuwako kwake. Basi wewe unapaswa kuwa katika umbali wa kuweza kuongea na Yesu, wala usiwe na wasi wasi juu ya kusema maneno yaliyo sahihi. Ongea tu naye kwa unyofu wa moyo na bila kuficha kitu. Ongea juu ya kila kitu. Yeye amepitia maumivu makali sana ya kifo kile chenyewe ili apate kuwa Msiri wako.
2. Jinsi Ya Kuomba

Tufundishe sisi kuomba.
"Baba yetu uliye mbinguni, jina lako litukuzwe, ufalme wako uje, mapenzi yako yatimizwe hapa duniani kama huko mbinguni. Utupe leo riziki yetu. Utusamehe deni zetu, kama sisi nasi tulivyowasamehe wadeni wetu. Wala usitutie majaribuni, lakini utuokoe na yule mwovu, kwa kuwa ufalme ni wako, na nguvu, na utukufu, hata milele. Amina" - (Mathayo 6:9-13).
Kulingana na mfano huo ambao Yesu aliutoa katika sala yake, sisi tunatakiwa kumwendea Mungu kama Baba yetu aliye mbinguni. Tumwombe kwamba mapenzi yake yatawale mioyo yetu kama vile mapenzi yake yanavyotawala katika mbingu yote. Tunamtafuta ili atupatie mahitaji yetu ya kimwili, msamaha wake, kwa ajili ya kuwa na roho ya kuwasamehe wengine.
Kumbukeni ya kwamba uwezo wetu wa kuipinga dhambi unatoka kwa Mungu. Sala ya Kristo inahitimisha kwa maneno ya sifa kwake.
Safari nyingine Yesu aliwafundisha wanafunzi wake kumwomba Baba "kwa jina langu" (Yohana 16:23) - yaani, kuomba kulingana na kanuni zake Yesu. Hii ndiyo maana Wakristo kwa kawaida hufunga sala zao kwa maneno haya: "Katika jina la Yesu, Amina." Amen (amina) ni neno la Kiebrania limaanishalo "Na iwe hivyo".
Japokuwa sala ya Bwana inatoa mwongozo juu ya mambo tunayotakiwa kuyaomba na jinsi ya kutunga sala, mawasiliano yetu na Mungu yanakuwa bora sana kama yanatoka moyoni mwetu kwa hiari.
Tunaweza kuomba juu ya kila kitu. Mungu anataka tumwombe msamaha kwa dhambi zetu (1Yohana 1:9), tumwombe atuongezee imani (Marko 9:24), tumwombe uponyaji wa maumivu na magonjwa yetu (Yakobo 5:15), na kumwagiwa kwa Roho (Zakaria 10:1). Yesu anatuthibitishia kwamba tunaweza kumpelekea yeye mahitaji yetu yote, pamoja na mashaka yetu; mno kuweza kumwomba.
("Mwekeeni matatizo yenu yote, maana yeye anawatunzeni") - 1 Petro 5:7.
Mwokozi wetu anapendezwa na mambo yo yote madogo yahusuyo maisha yetu. Moyo wake huchangamka wakati inapomwendea mioyo yetu kwa upendo na imani.
3. Maombi Ya Faragha

Tuombapo, Yesu, Kuhani wetu Mkuu, yu karibu nasi kutusaidia:
"Tunaye mmoja ALIYEJARIBIWA KWA KILA NJIA, KAMA SISI TUNAVYOJARIBIWA -lakini alikuwa hana dhambi. Basi na tukikaribie kiti cha neema kwa ujasiri, ili tupate kupokea rehema na kupata neema ya kutusaidia wakati wa mahitaji" - (Waebrania 4:15,16).
Je, una wasi wasi, mfadhaiko, hatia? Weka hayo mbele zake Bwana. Ndipo yeye anaweza kukidhi kila hitaji tulilo nalo.
Je, ni lazima tuwe na mahali maalumu pa maombi hayo ya faragha?
"wewe unaposali, ingia katika chumba chako, funga mlango na kumwomba Baba yako, ambaye.. atakujazi." - Mathayo 6:6.
Zaidi ya kuomba wakati wa kutembea mitaani, kufanya kazi, au kufurahia mkutano fulani, kila Mkristo angekuwa na muda fulani uliotengwa kila siku kwa maombi yake yeye peke yake pamoja na kujifunza Biblia. Tunza miadi yako ya kila siku na Mungu wako wakati unapokuwa mchangamfu sana na wakati unapokuwa makini sana.
4. Maombi Ya Hadhara

"Kwa kuwa wawili au watatu wanapokusanyika pamoja katika jina langu, nipo pamoja nao pale." - Mathayo 18:20.
Mojawapo ya mambo makuu kuliko yote tuwezayo kufanya sisi kama familia ni kukuza maisha ya maombi ya pamoja. Waonyesheni watoto kwamba tunaweza kupeleka mahitaji yetu kwake moja kwa moja. Watakuwa na msisimko juu ya Mungu watakapoona anajibu maombi yanayohusu mambo halisi ya maisha yao. Ifanyeni ibada ya familia kuwa wakati wa furaha na kubadilishana uzoefu wa maisha katika hali ya uhuru.
5. Siri Saba Za Maombi Yanayojibiwa
Musa alipoomba, Bahari ya Shamu iligawanyika. Eliya alipoomba, moto ulishuka kutoka mbinguni. Danieli alipoomba, malaika aliyafumba makanwa ya simba wale wenye njaa kali. Biblia inatueleza visa vingi vya kusisimua vya maombi yaliyojibiwa. Tena inapendekeza kwetu maombi kama njia ya kupata ule uweza kwetu maombi kama njia ya kupata ule uweza mkuu wa Mungu. Yesu anaahidi hivi:
"Mkiniomba neno lo lote kwa jina langu, nami nitalifanya" - (Yohana 14:14).
Lakini maombi mengine bado yanaonekana kana kwamba hayasikilizwi. Kwa nini? Hapa chini zipo kanuni saba zitakazokusaidia wewe kuomba kwa ufanisi zaidi:
(1) Uwe karibu sana na Kristo.
"NINYI MKIKAA NDANI YANGU, na maneno yangu yakikaa ndani yenu, ombeni mtakalo lote nanyi mtapewa." - Yohana 15:7.
Tunapoupa kipaumbele uhusiano wetu na Mungu na kuwa karibu naye, tutakuwa tunasikiliza na kutazamia kupata majibu kwa maombi yetu ambayo, vinginevyo, tusingeyatambua.
(2) Endelea Kumtumaini Mungu.
"MKIAMINI, mtapokea yote myaombayo katika sala zenu" - (Mathayo 21:22).
Kuamini au kuwa na imani, maana yake ni kwamba tunamtazamia Baba yetu aliye mbinguni kwamba kweli atatupa hayo mahitaji yetu. Kama wewe una wasiwasi kwamba huna imani, basi, kumbuka kwamba Mwokozi alitenda mwujiza kwa mtu yule aliyemsihi sana akiwa amekata tamaa, aliyesema:"
"Naamini, nisaidie kutokuamini kwangu!" - (Marko 9:24).
Wewe kazana tu kuitumia imani ULIYO nayo; usiwe na waiswasi juu ya imani ile usiyo nayo.
(3) Jisalimishe kimya kimya chini ya mapenzi ya Mungu.
"Huu ndio ujasiri tulio nao kwake, ya kuwa, tukiomba kitu cho chote SAWA SAWA NA MAPENZI YAKE, anatusikia" - (1 Yohana 5:14).

Roho Mtakatifu atakusaidia kulenga shabaha yenyewe: "Roho anawaombea watakatifu kulingana na mapenzi ya Mungu" (Warumi 8:27. Kumbuka kwamba mapenzi yetu yangeweza kulandana siku zote na mapenzi ya Mungu endapo sisi tungeweza kuona kama yeye anavyoona.
(4) Mngojee Mungu kwa Saburi.
"NALIMNGOJA BWANA KWA SABURI, akaniinamia akakisikia kilio changu" - (Zaburi 40:1).
Jambo kubwa hapo ni kukaza mawazo yako yote kwa Mungu, kukaza mawazo yako yote juu ya suluhisho lake. Wala usithubutu kumwomba Mungu akusaidie kwa dakika moja, na halafu kujaribu kuzizamisha shida zako kwa kujifurahisha katika anasa dakika inayofuata. Umngoje Bwana kwa saburi; tunahitaji kuwa na nidhamu hiyo vibaya sana.
(5) Usiing'ang'anie Dhambi iwayo yote.
("Kama ningalinuia maovu moyoni, Mwenyezi-Mungu hangalinisikiliza")- Zaburi 66:18.
Dhambi ijulikanayo hukata mara moja uweza wa Mungu katika maisha yetu; inatutenga mbali na Mungu (Isaya 59:1-2). Huwezi kuishika na kuing'ang'ania dhambi kwa mkono mmoja na kunyosha mkono mwingine kupokea msaada wa Mungu. Ungamo la dhambi litokalo moyoni hasa pamoja na toba ya kweli ndilo suluhisho la tatizo hilo.
Kama sisi hatutaki kumruhusu Mungu kutuweka huru mbali na mawazo, maneno na matendo yetu mabaya, basi, maombi yetu hayawezi kutuletea jibu lo lote.
"Hata mwaomba, wala hampati, kwa sababu mwaomba vibaya, ili mvitumie kwa tamaa zenu" - (Yakobo 4:3).
Mungu hatajibu "ndiyo" kwa maombi ya uchoyo. Acha wazi masikio yako yapate kuisikia sheria ya Mungu [Amri Kumi], yaani, mapenzi yake, naye ataacha masikio yake wazi kuzisikia dua zako.
"Yeye aligeuzaye sikio lake asiisikie sheria [Amri Kumi], hata sala yake ni chukizo" - (Mithali 28:9).
(6) Tambua Kwamba Unamhitaji Mungu.
Mungu huwajibu wale wanaoomba kuwako kwake na uweza wake katika maisha yao.
"Heri wenye njaa na kiu ya haki, maana hao watashibishwa." - Mathayo 5:6.
(7) Kuendelea Kuomba Tu.
Yesu alitoa kielelezo cha kuwapo kwa haja ya kuendelea tu kutoa dua zetu kwa kusimulia kisa kile cha mjane aliyekuwa anaendelea tu kuomba na kuendelea kuja kwa hakimu akiwa na ombi lake lile, lile. Mwishowe yule hakimu alisema, huku akiwa ameudhika vibaya sana, "Kwa kuwa mjane huyu ananiudhi, nitahakikisha kwamba nampatia haki yake." Kisha Yesu alitoa hitimisho lake hili: "Je! Mungu hatawapatia haki wateule wake wanaomlilia mchana na usiku? Je! atazidi kuahirisha kuwapatia haki yao?" (Luka 18:5-7).
Zungumza na Mungu juu ya mahitaji yako yote, matumaini yako yote, na ndoto zako zote. Omba mibaraka ya pekee, omba msaada unapokuwa na shida. Endelea kutafuta, tena endelea tu kusikiliza, mpaka ujifunze kitu fulani kutokana na jibu lake Mungu.
6. Malaika Wanayahudumia Mahitaji Ya Waombao

"Nalimtafuta BWANA akanijibu; akaniponya na hofu zangu zote... malaika wa BWANA hufanya kituo kuwazunguka wale wamchao na kuwaokoa" (Zaburi 34:4-7).
Tunapoomba, Mungu anawatuma malaika zake kujibu maombi yetu (Waebrania 1:14). Kila Mkristo anaye malaika wake mlinzi anayetembea pamoja naye:
"Angalieni msimdharau mmojawapo wa wadogo hawa. Kwa maana nawaambia ya kwamba MALAIKA WAO mbinguni siku zote huutazama uso wa Baba yangu aliye mbinguni." - Mathayo 18:10.
Kwa sababu ya maombi yetu tunayotoa:
"Bwana yu karibu. Msiwe na wasiwasi na jambo lo lote, lakini katika kila jambo kwa maombi na dua zetu pamoja na kushukuru, wekeni mambo yenu myatakayo mbele zake Mungu. Ndipo amani ya Mungu, ipitayo ufahamu wote, itawahifadhi mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu." - Wafilipi 4:5-7.
7. Mtindo Wa Maisha Ya Kikristo
Biblia inaeleza wazi juu ya mtindo wa maisha ya Kikristo. Kulingana na Waefeso 4: 22-24, Mkristo anatakiwa ku"vua" mtindo wake wa maisha ya zamani uliotokana na "tamaa zenye kudanganya", na ku"vaa" mtindo mpya wa maisha ambao ume"umbwa kwa mfano wa Mungu." Katika maandiko hayo na mwongozo tuligundua kwamba wakati ule wa kuzaliwa upya sisi tuna"umbwa upya" kuwa watu tofauti ndani ya Kristo.
Mwongozo huu na miongozo sita inayofuata hutangaza upya mtindo wa maisha ya Mkristo; huifunua siri ya maisha ya Kikristo yenye furaha. Itakusaidia wewe kujenga uhusiano wenye nguvu zaidi na Kristo, ambao matokeo yake yatakuwa mtindo wa maisha ya Kikristo ulio tofauti. Kwa hiyo kaza macho yako kwa Yesu leo hii, nawe unaweza kuwa na sehemu katika sherehe ile ya mwisho ya ushindi wakati amani yake Kristo itakapotawala bila kupingwa.
MADA YA KWANZA.
MAHUBIRI.
Malengo ya mada.
Baada ya kumaliza mada hii mwanafunzi
ataweza.
§ Kueleza maana
yamahubiri.
§ Kueleza maana
ya kuhubiri.
§ Kueleza wito
wa kuhubiri ulivyo.
§ Kueleza
umuhimu wa kujifunza homiletics.
A. UTANGULIZI
Katika kozi hii tutashughulikia mojawapo ya
kazi kuu ya kanisa.
Mojawapo ya
wajibu mkuu ambao umewekwa mikononi mwa kanisa ni kuhubiri ujumbe wa Mungu yaani Injili. 1Kor 1:21
a)
Ni amri iliyo wazi toka kwa Bwana Yesu kwa wafuasi wake. Mk 16:15.
“Enendeni ulimwenguni mwote
mkaihibiri Injili kwa kila kiumbe”.
b)
Kuhubiri ni mojawapo ya kazi ya
thamani sana
ambayo Mungu ametupa. Kuwa msemaji wa Mungu, yaani Mjumbe wa Kristo. 2Kor 5:20.
c)
Kuhubiri ni wajibu mkuu. Rumi
10:14-15.
d)
K wa njia ya mahubiri Mungu
alichagua kujidhihirisha mwenyewe kwa mwanadamu.
B. MAANA
YA MAHUBIRI.
Neno mahubiri
linatokana na maneno mawili ya kigiriki ambayo ni homileo na homilia yenye
maana ya ‘kuwa pamoja na, kuongea na kuwasiliana.
a)
Homily pia humaanisha ujumbe au hotuba.
b)
Elimu inayohusu namna ya kuhubiri huitwa Homileticts.
c)
Homiletics ni ustadi wa
kuhutubia au kuhubiri.
d)
Mtaalamu wa elimu ya kuhuri huitwa Homilist
e)
Homiletics huhusisha kujifunza kila kitu kinachohusiana na ujuzi wa
kuhubiri au kutunga hotuba.
f)
Mahubiri huhusu kujifunza kila kitu kinachohusiana na ujuzi wa kuhubiri
masomo ya Biblia.
g)
Mahubiri ni ujuzi wa kuhubiri.
h)
Ni elimu au taaluma inayohusu kuhubiri Neno la Mungu.
i)
Ni elimu inayohusu namna ya kuhubiri.{ somo juu ya kila kitu
kinachohusiana na kuhubiri}.
j) Kuhubiri ni kutangaza ujumbe wa Mungu. Mungu
hutumia watu wake aliowachagua kuhubiri ujumbe wake.
k)
Ujumbe unapaswa kuwa ujumbe wa Mungu Kitu kingine chochote na ujum
si mahubiri ila ni maoni na falsafa
za kibinadamu tu.
l) Kuhubiri ni
lazima kuwe ni kutangaza binafsi na si kusoma au kuandika
a)
Dr. Martyn Lolyoyd Jones
alisema “ Wahubiri huzaliwa na
hawafanywi kamwe. Kamwe hutamfundisha mtu kuwa mhubiri kama
yeye si muhubiri. Lakini muhubiri wa kuzaliwa unaweza kumsaidia na kumwendeleza
akawa mhubiri bora kwa njia ya mafunzo”
b)
-Mhubiri si chanzo cha ujumbe.Mungu ndiye chanzo cha ujumbe na mhubiri
ni bomba au mfereji ambako Mungu hupitishia ujumbe wake kwenda kwa watu
aliowakusudia. Ujumbe wa Mugu hutiririka kupitia utu wa mhubiri.
c)
-Ujumbe unapaswa kutiririka kwa uhuru toka kwenye chanzo chake (Mungu)
kwenda kwa wakusudiwa yaani hadhira au wasikilizaji.
d)
Mahubiri ni zao la mambo mawili
ambayo ni Mungu na mhubiri.Mahubiri mazuri huzaliwa kutokana na
ushirikiano mzuri (umoja) na ushirika mzuri
kati ya Mungu na mhubiri.
Hivyo kuna
vipengele viwili vya wazi katika mahubiri S cha kwanza ni kile cha ki Mungu na
cha pili ni kile cha kibinadamu.
Kwa sababu ya
wito wake mkuu mhubiri anapaswa kuwa mwaminifu na awe na ufahamu wa kutosha juu ya Neno la Mungu.
C. MAANA YA KUHUBIRI.
Mahubiri yana
lengo mahususi katika mpango wa Mungu.
Ni njia mabayo kwayo Mungu
ameamua kuwafikia waliopotea dhambini na kuwaimarisha waamini.Kkwa sababu
mahubiri ni njia ya mungu kuwafikia
wanadamu tutatazama maana ya kuhubiri kwa mitazamo mbalimbali kama
ilivyo ainishwa na wataalamu wa masomo ya homiletics.
1.Kuhubiri ni kuielezea imani.
Mojawapo ya
malengo ya mahubiri ni kuelezea au kutangaza kweli za maandiko matakatifu. Kila
hotuba au ujumbe wapaswa kuwasilisha kweli za maandiko kwa njia itakayowezesha
hadhira kupata uelewa zaidi ju ya maandiko matakatifu.Kuhubiri husababisha
imani kuumbika kwa wasikilizaji wako. Hubiri kwa kukuza imani na kuielezea
imani katika mwana wa Mungu.
II. Kuhubiri ni kuitetea imani.
Haitoshi
kuelezea ukweli wa Mungu bali tunapaswa kuutetea. Shetani, ulimwngu na maadui
wa imani huvamia na kupotosha kweli za neno la Mungu. Hivyo ni lazima kwa
mhubiri yoyote kuwa tayari kuitete imani ya kweli kwa njia ya kuhubiri kweli za
ki-Biblia. Kuna wahubiri wengi wa uongo ambao kazi yao ni kuposha kwali za maandiko matakatifi.
Ni jukumu la kila mhubiri wa kweli kuhakikisha anasimama imara katika kuitetea
imani ya kweli.
III.Kuhubiri ni kuinjilisha.
Wajibu mkubwa wa
Mhubiri ni kuitangaza injili kwa watu waliopotea dhambini. Ni lazima watu wote
waliopotea wapelekewe injili ili wapte kutambua
hali yao
ya kupotea na kuongozwa kwenye wokovu wa Yesu Kristo.
IV. Kuhubiri ni kukemea dhambi.
Kama ukichunguza hotuba za agano jipya utagundua kwaqmba
hakuna mubiri hata mmoja aliyesita kukemea dhambi.mfano Yesu, Yohana, Paulo,
Petro n.k wote walikemea dhambi kwa nguvu zo katika kila mahubiri. Mhubiri
nilazima akemee dhambi kila mara kwani Mhubiri ni kinywa cha Mungu. Kemea dhambi
bila kuogopa chochote .
V. Kuhubiri ni kuhamasisha waamini.
Mahubiri
hutakiwa kuwasaidia wakristo kukua katika neema ya Mungu. Pamoja na kuonya na
kukemea dhambi mahubiri hutakiwa kuwahamasisha na kuwawezesha waaamini kukua
kiroho na kufikia kimo cha Kristo.
VI. Kuhubiri ni kufikia mahitaji ya
hadhira.
Mahubiri
yatakuwa yameafanikiwa kama yatakuwa
yamepokelewa na kukutana na mahitaji ya waikilizaji. Mhubiri kwa uangalifu
anatakiwa kujiweka katika daraja sawa na wasikilizaji. Anatakiwa kujitahidi
kuhakikisha unapokelewa na makutano na kukutana na mahitaji yao.
VII.Kuhubiri ni kudhihirisha uweza wa Mungu.
Bwana Yesu aliahidi kuwa na wahubiri kwa
kulithibitisha neno kwa ishara na maajabu. Popote injili inapohubiriwa ni
sharti Bwana awepo
akiithibitisha kwa
isharaMk 16:15,20. 1Kor 2:4
D.
WITO WA KUHUBIRI
Sehemu ya muhimu
sana katika
kuhubiri ni wito. Kimsingi wito ni wa mtu binafsi Mungu huwaita watu katika
huduma na watu hupokea hilo rohoni mwao kisha huja uthibitisho wa nje
kupitia kanisa au watumishi mbalimbali na fursa mbalimbali. Mungu Huwaita watu
wake katika nafasi na huduma mbalimbali. Wengine kuwa wachungaji, wamishenari,
wazee wa kanisani, wainjilisti, au huduma nyinginezo.
Kazi ya kuhubiri
si ajira ambayo mtu anakwenda chuoni kusoma kwa lengo la kupata baada ya kuhitimu masomo yake, bali ni mwito
mtakatifu ambao mtu huitwa na Mungu mwenyewe kuwa muhubiri.
Mtu huenda chuoni ili kupata maarifa
yatakayomwezesha na kumsaidia katika kutimiza mwito wa Mungu uliondani yake.
Haendi chuoni kupata mwito bali wito husababisha mtu kwenda chuoni kama sehemu
ya maandalio.
Hivyo wito
usichanganywe na ajira na maslahi binafsi ya mtu. Ni lazima wito uheshimiwe na
kuogopwa. Waamini hawapaswi kujihusisha na huduma kwa lengo la kujinufaisha na
kujipatia mali
kwa njia za ujanja ujanja.
Kimsingi kila
mwamini ni muhubiri kwani agizo kuu linamhusu kila mwamini. Kila mwamini
anapaswa kujihusisha na kupeleka injili kwa watu waliopotea dhambini hili ni
agazo la jumla.
Lakini kuna watu
maalum ambao Bwana ameweka wito wa muda
wote(Full time commitement) ndani yao.
Amewachagua kwa kusudi hili katika maisha yao
na muda wao wote. Hawa wanasimama katika zile huduma tano za uonozi katika
kanisa, ambao ni mitume, manabii, wainjilisti, wachungaji na waalimu. Hawa ndio
Bwana amewaweka kusimama katika kazi ya kuhubiri ya muda wote, Wao hawapaswi
kujihusisha na shughuli zingine bali kazi yao
ni kulihudumia Neno na kuomba yaani Kuhubiri. Bwana ameweka mwito mtakatifu
ndani yao ambao
ni wajibu mkuu na wa kuogofyapia{.Mdo6:2,4} hili ni agizo mahususi.
Wito huu
haupatikani kwa njia ya kusoma au kwa njia ya ulaghai bali kwa kuitwa na Mungu
mwenyewe kuwa msemaji wake. Kuna baadhi ya makanisa ambayo yameufanya wito wa
Mungu kuwa ni ajira. Kwani wao huwapeleka watu kwenda chuoni kusomea huduma
fulani mfano uinjilisti, uchungaji nakadharika kwao wito si jambo la msingi ila
elimu ndiyo yenye kupewa kipaumbele. Wao
humpa mtu kushika nafasi ya huduma baada
ya kuhitimu mafunzoya chuo cha Biblia bila kujali kama
ana wito au la.
Matokeo yake ni
kwamba makanisa yamekuwa yakiongozwa na kuhudumiwa na watu wasio na wito wenye
kutegemea elimu ya darasani tu, jambo ambalo ni hatari kwa maendeleo na uhai wa
kanisa.
Elimu ni jambo
la zuri sana
lakini elimu haiwezi kuchukua nafasi ya wito katika kanisa la Mungu ikiwa
tunataka kufikia kusudi la Mungu la mwito mtakatifu na kusimama kiuaminifu
mbele zake kupata ushindi mkuu.
Usiwe mtumwa wa
elimu. Elimu hii unayopata ikusaidie
katika kumtumikia Mungu na kufanya huduma lakini isichukue nafasi ya Roho
mtakatifu katika maisha yako na huduma yako. Wala haipaswi kuwa badala ya Roho
mtakatifu.
Usiongozwe na
elimu bali ongozwa na Roho mtkatifu.
Usihubiri kwa
maneno yenye hekima pekee kwa lengo la kushawishi akili za watu bali
hubiri Kwa dalili za Roho mtakatifu na nguvu. 1Kor 2:4.
Hakikisha
unautumikia wito ambao Mungu ameweka ndani yako kwa gharama yoyte ile bila
kujali mazingira au kitu kingine chochote.
Kwa hiyo wito wa
kuhubiri hautoki kwa mwanadamu yoyote
Yule bali toka kwa Mungu mwenyewe. Mungu huwafanya watu wake kuwa wahubiri.
Jiulize wewe ni
mhubiri wa kufanywa na nani ?
Kweli kuu
kuhusu wito wa kuwa mhubiri.
1. Roho mtakatifu huweka wito ndani ya mtu.
Wito wa Mungu huja juu ya mtu kupitia Roho
mtakatifu. Katika akili ya kawida ni kazi kubwa kuhubiri au kutumika. Wito huja
kwa watu wa aina zote na umri wote wowote. Baahi ya watu husikia wito na
kujitoa wangali wadogo lakini wengine katika umri mkubwa n.k
2. Shauku ya kutimiza wito.
Watu wanaoitwa
kuwa wahubiri waliumbwa na Mungu kwa kusudi hiloYer1:4-10
Hawawezi kupata
utoshelevu kwa kufanya kitu kingine chochote. Hawawezi kupinga kujihusisha
katika huduma au kuchukua fursaza kuhubiri. hHata kama
hakuna nafai za kutumika moja kwa moja
bado watatafuta nafasi katika huduma yoyote inayojitokeza.
3. Mungu huwaandaa wale anaowaita kwajili
ya huduma.
Mungu hawaiti
watu ambao hwana uwezo wa kutimiza mwito wake. Wahubiri wengi wanakipaji cha
kuongea. Watu wenye wito juu ya watoto hupewa
hupewa Mungu huwaandaa kwa kuwapa uwezo kwa kufanya huduma na watoto n
na wanaoitwa kuwa wacghungaji huqwezeshwa kuwa wachungaji. Popotye na kwa namna
yoyte Mungu huwaandaa na kutoas nguvu ya uwezesho juuv yao.
4. Wito wa Mungu wapaswakuwa wazi.
Wito wa Mungu
usifichwe. Wito wa Mungu ulioju yako wapaswa kuwa wazi kwa watu wangine lakini
haupaswi kukimbilia kwenye wito huo mara moja. Hutakuwa na furaha na mafanikio
na wito huo mpaka utakopokuwa umejisalimisha kwa mapenzi sahihi ya Mungu juu
yako.
5. Wito wa Mungu ni wito wa matayarisho.
Kuna wajibu
mwingi na mkubwa ambao huja pamoja na wito wa kuhubiri .Mungu akisha mwita mtu
humuandaa kwanza kabla ya kumtuma na kumwachilia kwnye huduma aliyomuitia.
Mhubiri anapaswa kujiimalisha kiroho na kimwenendo.Anatakiwa ajiandae kiakili
kwa kusoma na kupata mafunzo. Pia anapaswa kujiandaa kimatendo kwa kunuo vipawa
vilivyondani yake na kuyatisha maisha yake yote kulingana na wito ulio ndani ya
E.Umhuhimu wa kujifunza somo hili la homiletics.
a) Linatusaidia
kujua mbinu mbalimbali za kuhubiri.
b) Linatusaidia
jinsi ya kuhubiri bila kuwachosha watu.
c) Linatufanya kuwa
na ujasiri tunapohubiri.
d) Linatusaidia kuhubiri
kwa usahhi.
e) Linatusaidia
kutambua mahubiri ya uongo.
f) Linatusaidia
kujua nakuheshimu wito tulio nao.
g) Linatusaidia
kujua kusudi la Mungu la mahubiri.
Zoezi.
Jibu maswali fafuatayo. Wanafunzi waweza kujibu katika
makundi au mmoja mmoja kama kazi ya nyumbani
kwa kadri mwalimu atakavyoona inafaa.
1. eleza maana ya mahubi kwa mitazamo mbalimbali.
2.Eleza vile mahubiri
yasivyo.
3. Toa tofauti iliyopo
kati ya mahubiri na kuhubiri.
4. Taja faida tano za
kujifunza somo la kuandaa mahubiri.
5. Tathmini misukumo
mbalimbali inayosababisha watu waingie katika huduma tano za uongozi wa kanisa.
na hali hawana wito.
6.Eleza namna gani mtu
aweza kujua kwamba Mungu anamwita kuingia katika huduma.
7.Eleza umuhimu wa
kindicha maandalizi na matayarisho kabla yam tub kuingia katika huduma ambayo
Mungu anamwita kuifanya.
8. Jadili kauli
inayosema wito wa Mungu ni wito wa matayarisho.
9. jadili usemi
unaosema kwamba Mungu humuanda mtu aliyemwita kabla ya kumwachilia katika
huduma.
10. Jadili mabo ya
msingi kuzingatia katika kipindi cha matayarisho kwajili ya huduma na wito ambao Mungu ameweka ndani yako.
MADA YA TATU: MBINU ZA UTAYARISHAJI WA MAHUBIRI.
Utngulizi
Katika mada hii tutajadili aina
mbalimbaliza utayarishaji wa mahubiri, maeno ya mahubiri na sehumu za mahubiri
au hotuba. Tutapitia kwa undani kla kimojawapo ili kujifunza jinsi vipengele
hivyo jinsi vinavyohusiana na amhubiri tunavyoweza kuvitumia katika huduma ya
kuhubiri na kuandaa mahubiri.
Malengo ya mada.
Baada ya kumaliza kujifunza mada hii mwanafunzi ataweza.
Kutambua njia na mbinu mbalimbaliza
utayarishaji wa ujmbe au hotuba.
Kuandaa mahubiri kwa kutmia mbinu
mbalimbali.
Kutambua sehemu tatu za mahubiri au hotuba.
A.
Utayarishaji Wa Somo.
Kuna aina nyingi
za utayarishaji wa somo au hotuba, na kila mojawapo ina umuhimu wake. Lakini
katika mada hii tutajifunza aina tatu za utayarishaji wa somo au hotuba.
Kila mwanafunzi
anatakiwa kuelewa aina zota tatu na anapaswa
kujizoeza kutumia njia hizi zote ili aweze kufaidika zaidi.
1. SOMO LILILOANDIKWA.
Katika aina hii
mhubiri hupaswa kuandika ila kitu anachokusudia kukihubiri. Wakati
mwingine somo lote huandikwa. Kilac eneo
la asomo huchambuliwa kwa undani na kuwekwa katika maandishi. Ujumbe au somo
lote huandikwa kikamilifu kabla ya kuhubiri.
Mhubiri huelezea
kwa undani somo lake
anapohubiri likiwa katika
maandishi. Mhubiri anapohubiri mara nyingi hupitia kila kitu alichokiweka
katika maandishi.
Faida za aina mbinu hii.
a)
Ujumbe wote huandaliwa kwa uangalifu mkubwa.
b)
Ujumbe huwasilishwa kwa umakini na uhalisia.
c)
Ujumbe huwa ni wa kitaalam.
d)
Mhubiri hujikita katika somo.
Hasara ya mbinu hii.
a)
Somo huwa haliwavutii wasikilizaji.
b)
Utoaji wa ujumbe wa namna hii unaweza kuwa wa kuchosha usipofanywa kwa
uangalifu.
c)
Utayarishaji wake huhitaji muda mwingi.
2.SOMO LISILOANDIKWA.
Hii ni mbinu ya
utayarishaji wa somo bila kuliandika. Mhubiri huosma vifungu vya maandiko na
kivitafakari kwa kina kisha hukariri vitu vya msingi vilivyo katika ujumbe wake
na maandiko yanayohusika.
Aina
hii mara nyingi hutumika katika kutayarisha na kuhubiri ujumbe wenye uvuvio
zaidi. Ujumbe hutiririka toka rohoni na huwa wa kuvutia mno.
Faidaza mbinu hii.
a)
Ni rahisi kutmia.
b)
Haihitaji muda mwingi wa matayarisho.
c)
Mhubiri huwa huru kutoa kila kinachokuja ndani yake maadam kinaendana na
ujumbe wa somo.
d)
Huwasisimua wasikilizaji na kuwavutia.
Udhaifu wa mbinu hii.
a)
Mhubiri kutoka nje ya ujumbe wake hasa ikifanywa na mhubiri asiye na
uzoefu.
b)
Wasikilizaji waweza kulielewa somo vibaya. (waweza kuelewa vile somo lisichomaanisha).
c)
Somo kutowajenga wasilizaji na kuishia kusisimua tu akili zao.
d)
Somo kutokuwa na maana halisi na hivyo kutowajenga wasikilizaji.
3.MBINU YA SKELETONI.
Njia hii
huhusisha kuandika maelezo ya somo au ujumbe kwa kifupi kwa lengo la
kufanikisha utunzaji wa kumbukumbu sahihi
juu ya ujumbe au somo.
Kwa maana
nyingine ni kwamba mhubiri hutayarisha muhtasari wa ujumbe au somo.Mhutasari
huo huwa kama skeleton ya somo mfano wa fuvu
la binadamu.
Mhubiri huhubiri
kwa kutumia skeleton hiyo. Kazi yake hasa ni kuweka nyama katika skeleton hiyo
kwa njia ya mahubiri. Hivyo anapohubiri huweka nyama katika mahubiri yake ili
yawze kuwa kitu kamili
. Mhutasari wa
somo huwa kama mifupa ya ujumbe. Ndiyo mifupa
mabayo huleta sura na mategemeo kwa kile mhubiri anachotamani kusema. Anavyosema
anaweka nyama katika mifupa na
kuufanya mwili wa somo lake. Hupanua mawazo yake ambayo maelezo yake mafupi yamekuza.
Faida za mbinnu hii.
a)
Mbinu hii humpa mhuburi uhuruzaidi.
b)
Utoaji wa somo huwa wa kuvutia sana.
c)
Somo huwajenga wasikilizaji bila kuwachosha.
d)
Mhubiri huweza kutoa somo kwqa mtiririko mzuri na sahihi.
Maeneo
ya mahubiri.
Kuna maeneo
makuu manne ambyo mahubiri huhusisha. Mhubiri yoyote ni lazima azingatie maeneo
hayo ili aweze kufanikisha mahubiri yake.
I.Wazo
. Hii huhusu
namna ya kupokea kichwa cha somo au ujmbe. Ni ujuzi unaohusu namna ya kupokea
ujumbe toka kwa Mungu. Huhusu namna ya kuptata wazo la awali na kichwa cha somo.
Mugu hupanda
mbeguya wazo kuhusu somo au ujumbe siku kadhaa kabla ya mahubiri. Mbegu hiyo
kukua kwa njia ya kuitafakari na maombi zaidi. Kutokana na ujuzi mhubiri
aweza kuuujenga uwezo wa kumbua mstari.
Muhubiri hupaswa
kuliemneleza na kulikuza wazo lililopandwa ndai yake kwa njia ya maombi,
kutafakari na kuchunguza zaidi juu ya wazo hilo ili aweze kutayarisha ujumbe.
Pata muda wa
utulivu utulie uweponi na omba nuru zaidi ya ufunuo huo.
II.Muundo.
Muundo huhusisha
uchambuzi wa wazo ili kuweza kugundua
kweli zilizomo katika wazo hilo.Baada ya kupokea Wazo toka kwa Mungu unapaswa
uanze kulichambua ili kutambua vitu
ambavyo wazo hilo
linavyo.
Katika hatua hii
inapaswa kuorodhesha kwa urahisi kila kitu kilichomo kwenye wazo hilo.Mara
nyingi unapokuwa katka hatua hii unahitaji kuandikwa kwa haraka ili kupata kwa
kifupi mtririko wa uvuvio unaokuja. Hakikisha kwamba unaaandika kila kitu. Ili uweze kuchambua baadae.
Ujenzi.
Huhusiha
kukusaya na kuayaweka mawazo yako uliyoyachambua katika kipengele cha uchambuzi
katika mpango mzuri. Kuweka kila kitu katika mpangilio mzuri kutakusaidia na kukurahisishia
katika utoaji wa somo lako. Kuwasislisha
mawazo yaliyoendelezwa hufanyika msaada sana
kwa wasikilizaji wako katika kuelewa na kufuata mpango wako wa kufikiri.
Somo
likiwalimechanganywa itawawia vigumu wasikilizaji wako katika kulielewa somo
hilo.Ujenzi wa osmo hulenga kulifanya somo rahisi kiasi cha kueleweka vizuiri
na wasikilizaji.
Ni muhimu sana kwa mhubiri kuliweka
somo katika namna itakayofanya lieleweke
kwa urahisi.
Mawasiliano.
Hii huhusu
namana mhubiri anavyowaislisha somo au
ujmbe kwa hadhira. Mhubiri anatakiwa
kuliwasilisha somo lake
kwa njia rahisi na
nyepesi kueleweka na waikilizaji wake. Anatak
a)
Kuwasilisha ukweli uliowazi na wenye kueleweka.
b)
Kuota ujumbe kwa njia ya kuteka akili za hadhira.
c)
Kuendeleza mawazoyako katika mpango ambao hadhira wataweza kuyafuata kwa
urahisi.
d)
Kuwahamasisha hadhira kulitendea
kazi somo. Yak 1:22.
B. Sehemmu Kuu
za Mahubiri na Hotuba.
Kwa
kawaida mahubiri au hotuba yoyote ile ni lazima iwe na sehemtu tatu ambazo kwa
pamoja huunda hotuba au mahubiri hayo.
Sehemu tatu hizo ni utangulizi, kiini na
hitimisho.Kila sehemu ni muhimusana na inatikwa kupewa uzito wake.
Sehemu
mojawapo ikipuzwa yawza kuvuruga au kuharibu kabisa ujumbe au hotuba yako.
I. Utangulizi
. Hii ni sehemu
ya kwanza ya hotuba. Utangulizi hutambulisha hotbuba au somo zima na kutoa
picha jinsi somo litakavyokuwa. Utangulizi ni sehemu muhimu ya ujmbe na kama hadhira hawajakusikilza kwa umakini katika kipindi
hiki cha awali yawezekana kutokuuelewa ujmbe wako au kutokukusikiliza vizuri
katika sehemu zinazobaki za hotuba yako.
Mara nygingi
utangulizi huwa kama muhtasari wa
ujumbe.Katika utangulizi mhubiri huwaeleza hadhira kwa kifupi juu ya kile
ulichopanga kuongelea au kuhubiri.
Mambo ya msingi katika uangulizi.
a)
Kuteka usikivu. utangulizi wako unapaswa utawale hamu na
mawazo ya wasikilizaji.
b)
Kujenga masikilizano. Lazima
ujenge mawasiliano kati yako na wasikilizaji.
c)
Kuleta kukubalika. Ni lazima
utangulizi kwako ukujengee kukubalika kwa wasikilizaji.
a.
Unapaswa kupata usikivu wao, matumaini na heshima.
d)
Kujulisha. Utangulizi wako unapaswa kuwaeleza
wasikilizaji kwamba somo lako lina husu nini hasa, na jinsi
utakavyoliwasilisha.
e)
Kusadikisha. Ni lazima utangulizi uwasadikishe wasilizaji
juu ya umuhimu wa ujumbe na kupata usikivu mzuri wa sehemu iliyobaki ya hotuba
yako.
f)
Usitoe utangulizi kwa kuomba msamaha. Usiseme “Bahati mbaya sikujiandaa
vizuri”
a.
Kufanya hivyo kutapoteza usikivu wa wasikilizaji wako na kukufanya
usiaminike kwao.
Sifa za utangulizi mzuri.
a) Sio wa kishindo mno. Utangulizi uwe wa kiasi usiweke hatua ambayo huwezi
kuifikia.
b) Sio mrefu mno. Kumbuka kwamba
utangulizi si ujumbe wote bali ni sehemu tu hivyo unapaswa kuwa mfupi.
c) Utangulizi uendane na ujumbe.
Utangulizi ni sharti ulenge kichwa cha somo. Waweza kuwa mhtasari wa somo au
kisa ambacho kinaonesha ukweli wakile
ulichokusudia kuongelea.
d) Unapaswa kuandaliwa kwa uangalifu.
Kwa sababu utangulizi wako ni kitu muhimu katika kuvuta usikivu wa hadhira
unapaswa kuandaliwa kwa umakini sana.
Tayarisha
utangulizi wako kwa kujiuliza maswali yafuatayo
a) “ Ningekuwa ni msikilizaji ujmbe huu nini kingenitvuta zaidi ili kuleta
usikivu katika yote niliyokusudia kuyasema?
b) “ Ni jambo gani hasa ambalo lngekaata
usikivu wangu?
Majibu yake unayoyapata ndiyo waweza
kuyatumiak katika sehemu ya utangulizi wa ujumbe wako.
Utoe nafasi ya
kuptia kwenye kiini cha ujumbe. Utangulizi unapaswa kutoa njia ya kupitia
kwenda kwenye kiini cha ujumbe. Kusiwe na pengo kati ya utangulizi na kiini cha
ujumbe.
2.Kiini.
Hiini sehemu kuu ya somo au
ujmbe ambayo imebeba ukweli wote wa somo. Hatua ya kwaza kwenye kiini ni kutoa
sekeletoni ya kiini na kisha hatua ya
pili ni kuweka nyama katika skeletoni
yako.Waweza kuweka nyama katika sekeletoni yako kwa kufanya yafuatayo:
Kufafanua misamiati mbalimbali inayojitokeza kwenye
kiini na kutoa maelezo ya dondoo ulizoziandaa. Tumia kamusi au itifaki ya
Biblia katika kupata maana ya maneno hayo.
Kutumia
vielelezso. Unapaswa kutumia vielelezo mbalimbali vitakavyosaidia katika
kulielezea somo lako au ujmbe wako.
Waweza kutumia
vielelezo vifuatavyo katika kulielezea na kufafanua ujumbe wako.
Vielelezo
binafsi.
Wahusika
mbalimbali katika Biblia wanaoweza
kutumika katika kuelezea dondoo zako. Ukweli wa kitaalam mfano
sayansi,historia, uvumbuzi, Tiba. n.k
Hadithi zenye
kufafanua somo lako.Usiwaachie hadhira kutoa fasili ya bali ifafanue mwenyewe.
Unapaswa
kukigawa kiini katika dondoo kwa kufuata mtiririko wa mawazo. Hubiri kwa
kufuata mtiririko wa mawazo wa kimantiki.
3.Hitimisho.
Hii ni sehemu ya mwisho ya hotuba au ujmbe
lakini kipengele cha muhumi sana
. Kipengele hiki kisipozingatiwa maana na malengo yote ya kuhubiri huvurugika
na kutokuwa na maana. Hivyo ni lazima kipewe uzito unaostahili.
Mambo ya
kuzingatia.
Tunia muda
kidogo kwa kuuelezea ujmbe kwa kifupi. Kazia maeneo ya msingi unayofikiri
kwamba hayakueleweka vizuri kwa hadhira
wakati ukuhubiri na yale yanayotakiwa kupewa uzito maalumu.
Pia waweza
kurudia kuzitamka kwa sauti dondoo za
ujumbe wako kila moja.
Usiwachushe(bore) kwa kuanza kurudia kuhubiri ujumbe wako wote.
Mwaliko.
Mwaliko ni
kipengele muhimu sana katika hitimisho. Kwa sababu mahubiri ni
tofauti na iana nyingine za hotuba hivyo mwaliko huwa ni muhimu sana kwa kuwa mahubiri huhusu kuchukua maamuzi au hatua juu
ya kile kilichohubiriwa. Mahubiri blia mwaliko huwa hayajafikia lengo la
kuhubiri. Mwaliko ni lazima katika mahubiri ya aina yoyote ile.
Mwaliko
huwa ni wakati wa kuitikia Kile Mungu amesema kupitia mahubiri. Ni
wakati wa kutendea kazi kile kilichofundishwa au kuhubiriwa.
Mhubiri anapaswa
kuufanya mwaliko kuwa wazi kwa wasikilizaji wote. Lengo la mwaliko si kuwaita
watu madhabahuni tu bali ni kuwahamasisha watu kuweka ujumbe katika
matendo.
Pia Mhubiri
hutakiwa kuuweka ujumbe wake katika matendo.
1.
Ukihubiri uponyaji waite watu madhabahuni na waombee uponyaji.
2.
Kuhubiri kutembea katika mamlaka unatakiwa udhihishe mamlaka hiyo.
3.
Ukihubiri utoaji waite watu kumtolea Mungu.
4.
Ukihibiri toba unapaswa kuwaongoza hadhira kwenye maombi ya toba na
kuwaita madhabahuni wale wanohitaji kutengeneza kwa upya mwenendo na mahusiano na Mungu na kuomba nao.
Wapeleke watu
kwenye matendo na matumizi Mt 21:23. Yak 2:22.
Unatakiwa
kuwaongoza hadhira kuomba kwaajili ya
ujumbe au somo kwa kadri ya maongozi ya Mungu na kwa kadri Mungu alivyosema na
kila mmoja.
Unaweza
kuwaongoza watu waimbe wimbo unaoendana na ujumbe uili kuwaogeza uweponi na
kuwapa hamasa.
Toa mwaliko kwa
watu ambao wanataka kuokoka na kama wapo omba
pamoja nao.
Baada ya hapo maliza na mkabiribishe
anaehusika na ratiba inayofuata.
Kwa kuhitimisha juu ya sehemu tatu za ujumbe
au hotuba twaweza kuvifupisha vipenele vyote hivyo vitatu kwa sentensi tatu
ambazo ni:
1.
Waambie hadhira kile unachotaka kuhubiri.(Utangulizi.)
2.
Hubiri kile ulichowaambia
(Kiini), kisha:
3.
Waambie kile
ulichohubiri.(Hitimisho).
AINA MBALIMBALI ZA MAHUBIRI.
I.
MAHUBIRI YA KIFUNGU.
Aina hii ya mahubiri hujengwa juu ya kifungu
kimoja kidogo cha maandiko tu.
Huhusisha kuchagua maelezo fulani maalum
ya maandiko na kuyachunguza, kuchambua na kugungua kweli zote zilizomo ndani
yake na kuziwasilisha kwa waikilizaji kwa mtindo rahisi na wenye kueleweka.
A. Faida za mahubiri ya Kifungu.
a)
Huvutia.
b)
Huzuia kutoka nje ya somo.
c)
Hufanya mahubiri kuwa ya ki- Biblia.
d)
Humwongezea mhubiri ujasiri.
e)
Husaidia wasikilizaji kulikumbuka
somo.
B. Jinsi ya kuandaa mahubiri
ya kifungu.Kuna mambo kadha ambayo
mhubiri anapaswa kuyazingatia wakati wa kuandaa mahibiri ya aya badhi ya mambo
hayo yamejadiliwa hapa chini.
1.Soma Biblia mara kwa mara. Unapaswa
kusoma Biblia mara kwa mara ikiwa unataka kuwa mhubiri mqwenye mafanikio katika
huduma yako.
-Tenga muda wa kusoma biblia kila siku.
Beba Biblia ndogo kila mahali unapokwenda ili upatapo mua uweze kuisoma.
2. Jifunze Biblia. Kujifunza ni zaidi
ya kusoma.Kujifunza kuna husiha kusoma Biblia kwa undani kwa kuchunguza
kikamilifu kila kitu kilicha katika maandiko unayosoma na kutafakari kwa
kina,.Yos1:8.
Unapaswa
kutafakari kwa uangalifu vitu unavyosoma. Viweke kwenye akiliyako na kuvifikiri
tena na tena.
Unapaswa
kujizoesha kuchambua kile ulichojifunza. Baada ya kukichambua kwa umakini
unapaswa kukiweka tena akilini.
2. Kuwa na Daftari la kuandikia. Kila
usomapo Biblia yako jitahidi kuwa na kalamu na daftari la kuandika mambo muhimu
un ayo jifunza.Jenga mazoea ya kuandika kwa ufupikila ufunuo unaoupata.
3. Dumisha hali ya maombi. Unapaswa kuwa katika hali ya maombi kila
usomapo Biblia.Omba Mungu akufunulie upate kulielewa Neno lake.Pia unapaswa
kumwomba Mungu akupe usikivu juu ya
kweli anazokufunulia katika Neno lake.
4. Jenga usikivu.Unapaswa kuwa katika
hali ya utulivu na usikivu katika nyanjazote yaani kimwili, kiroho na
kisaikolojia. Mungu hutoa ufunuo wake
kwa sauti ya kimya ndani ya roho ya mhibiri. Kama
hunautulivu na usikivu wa kutosha ni vigumu kugundua maarifa hayo..
-
C.Sifa za aya ya mahubiri
Kifungu cha mahubiri au
aya yapasa kuwa :
a. Yenye mamlaka ya ki-Biblia.
Mafundisho anayokusudia kuhubiri toka kifungu au aya fualni ya maandiko
yapasa ikubaliane na ile biblia nzima inachofundisha.
Katika
mahubiri ya kifungu kuna uwezekano wa kuchukua kimakosamstari nje ya maana yake
na kuutumia kufundishia kitu ambacho Biblia haikubaliani nacho.
Ni Muhimu sana kwa ,uhubiri kujua jinsi mstari
anaoshughulikia jinsi unavyokubaliana na kusudi la sura yote na kitabu chote.
Daima
mhubiri anapaswa kujitahidi kufasili aya yake katika nuru ya yale ambayo Biblia nzima inafundisha.
b.Kamili. Aya yapaswa kuwa katika maandisha ya ukweli
ulio kamilika.
Baadhi ya wahubiri huchukua kifungu cha
maneno katika mstari na kukitumia bila kujali maneno yaliyotangulia au
yanayofuata. Jambo hili si zuri na huzaa mafundsho ya uongo. Na huku
huitwa. “Kulichanganya neno la Mungu na
uongo……..2Kor 4:2.
Ni
lazima uepuke jambo hili kwani litaleta kutokuaminika na maelezo yasiyo ya ki-
Biblia na hatimae utawapotosha wasikilizaji wako.
c. Fupi kiasi. Kifungu cha mahubiri
chapaswa kitolewe kwenye maelezo ya maandiko ambayo ni mafupi nay a kulizisha.
c. Ya kueleweka. Aya yapaswa kueleweka
na iwe muhtasari wa kutosha wa kile unachotaka kukishirikisha.
*Unapaswa
ubaki katika mipaka ya kile ambacho aya yako inaelezea.
D. Namna ya kuandaa mahibiri ya aya.
a.
Elewa maneno yake vema.Kipitie kifungu kwa kukisoma mara kadhaa, kitafakari na
kujenga kumbukumbu juu yake na kiseme mwenyewe kwako. Hakikisha unakielewa
vizuri.
b. Elewa lugha yake.Tamabua lugha yake
kama ina maana halisi au kama ni lugha ya
mifanotu.
Jiulize
kama mwandishi alikuwa na maana hasaya
kile alichokiandika au maneno yake
yachukuliwe kama mfano wa mahubiri?
c.Changanua ujumbe wake.Chambua uhjumbe
unaoupata na kuutenga katika sehemu kadhaa zenye kulandana ili uweze
kuuwasilisha kwa mtiririko mzuri.
d. Chunguza maneno yake. Jitahidi
kugundua kile maneno hayo yalikusudia kuwasilisha hapo awali. Ikiwa una kamusi
ya kigiriki au Kiebrania unapaswa kulitazama neno hilo kwa lugha ya zamani au Kigiriki. Jaribi
kubaini kama kuna maana maalumu ndani ya mneno
unalolishughulikia.
Kufanya
hivyo kutakusaidia kugundua maaana yoyote maalumu ambayo mwandishi alikusudia
kuiwasilisha.
e. Tathmni mwendelezo wake. Baini
kweli zile mwandishi alitaka
kuzielezea. Tambua jinsi alivyo kamilisha katika kuziwasilisha kweli
hizo.
Jaribu
kufuata mwongozo wake na kuuendeleza
katika mtindo huo.
f. Mkutadha wa kifungu..
i.Maneno ya mbele nay a nyuma ya kifungu.
Angalia jinsi mistari iliyotangulia na inayofuata inachosema. Chunguza aya
kushusiana na sura nzima ambayo umetoka. Chunguza kifungu hicho katika nuru ya
kitabu kizima ambamo kinapatikana.
Jifunze kiini na mazingira yote ya kitabu.
ii. Hali ya mila. Je mila za wakati ule ziliathiri kile
kilichoandikwa? Je watu walioandikiwa kifungu hicho awali wangekuwa na wazo la
kile kilichoandikwa tofauti na ambalo tungepata katika hali yetu? Kama ndivyo nini ingekuwa maana inayolingana na sasa?
ii. Hali ya kihistoria. Je jambo hili
liliandikwa lini?je wakati huo ulishawishi kile kilichoandikwa? Je matukio ya
kwakati ule yaliyokuwa yakijulikana wakati ule wa uandishi yalikuwa na maana maalum ju ya kile kilichosemwa?
iv.
Hali ya kijiografia.
Mwandishi alikuwa wapi wakati anaandika maneno hayo?je Watu
walioandikiwa walikuwa wapi?Je mazingira yao
yana uhusiano wa chochote katika kle kilichosemwa?
v. Biblia kwa ujumla. Kila sehemu ya maandiko ifasiliwe kwa
uaminifu na kwa umakini ili ikubaliane na maandiko yote. Andiko lolote
lisifasiliwe nje ya mkutadha wake. Maandiko ni lazima yatafsiri maandiko.
E.Kupanga Maelezo.
Mpanglio
mzuru wa maelezo na kazi kwa ujumla ni
wa faida sana
kwa mhubiri. Hakikisha unapnga maelezo yako kimaantiki. Mpangilo mzuri wa kazi
na mawazo humwezesha mhubiri kulielewa vizuri somo na kulishughulikia somo
kikamilifu.
Pia
huwawezesha wasikilizaji kulielwa somo na kulikumbuka somo .
1.
Ujumbe uwe katika mpangilio.Panga
ujumbe wako katika mtiririko mzuri ili uweze kuufuata kwa urahisi wakati wa
kuhubiri.
2.
Weka ujumbe wako katika hali ya
kueleweka. Jitahidi kukamilisha vipengere vyote unavyohitaji kuviongelea
katika mahubiri yako. Kabla ya kupanda mimbarini.
3.
Kazia katika mawazo. Unapaswa
kuyaweka mawazo yakob katika sentensi fupi. Jifunze namna ya kuyaimarisha
mawazo yako kwa pamoja nakuyaelezea katika sentensi fupi zinazoeleweka kwa
urahisi.Jizoeze kupunguza na kulielezea wazo kwa sentensi moja.
4.
Tayarisha maelezo mafupi.Kumbuka
kwamba maelezo yako yako ili kusaidia kumbukumbu yako.unapaswa kuwa na vidokezo
vitakavyosaidia kulikumbuka somolako au ujumbe wako.
5.
Ufanye rahisi kuusoma. Ni
vizuri kupiga chapa mahubiri yako ili
uweze kusoma kwa urahisi wakati wa ukihubiri. Pia waweza kutoa vipeperushi na
vijarida kwa wasikilizaji wako ili waweze kufuatilia zaidi ujmbe au somo lako.
Zoezi.
1.
Eleza maana ya mahubiri ya aya.
2.Tathmini
ubora na udhaifu wa mahubiri ya aya.
3.Taja
mambo mengine muhuimu ya kuzingatia katika mahubiri ya aya au kifungu licha ya
yaliyotajwa katika kitabu hiki.
4.
Andaa hotuba ya mahubiri ya aya na kisha hubiri kwa dakika kumi mbele ya
wanafunzi wenzako.
II.
MAHUBIRI YA KUFAFANUA.
Mhubiri ya
kufafanua ni aina ya mahubiri ambaayo
huhusisha kuchagua sehemu kubwa ya maandiko na kuicghunguza kwa undani na
kuifasiri na kugungua kweli zilizomo katika sehemu hiyo ya maandiko na
kushirikisha mkutano au usharika wako.
Mfano unaweza
kuamua kupitia Injili yote ya Luka sura baada ya sura. Kuanzia sura ya kwanza,
unatafuta kufasili na kuelezea maana na umuhimu wake mstari kwa mstari sura kwa
sura mpaka umeimaliza yote.
Waweza
kushughulikia sura moja kila wiki, na baada ya wiki kadhaa utakuwa umemaliza
kitabu chote.Faida ya mahubiri ya ufafanuzi.
Hufanya mahubiri kuwa ya ki-Biblia.
1.
Yesu alitumia aina hii ya mahubiri. Alichukua kifungu cha Agano la kale
na kufasili maana yake kwa wasikilizaji wake.
2.
Petro alitumia njia hii siku ya Pentekoste.
3.
Stefano alitumia njia hii.
Huwezesha
waamini kuwa na msingi na uelewa mkubwa wa Biblia.Waamini huimalisha na huwa na
ufshsmu mzuri na wa kina wa Neno la Mungu. Kwani kweli zote zilizomo katika
kitabu kilichopitiwa tayari hufahamika vizuri kwa usharika wote.
Huvuta kuimalishwa na Roho mtakatifu.
Roho mtakatifu hulithibitisha neno lake
kwa ishara na miujiza
sawasawa na Kweli zote zilizofunuliwa katika kitabu husika.
Humfanya mhubiri kuwa wa ki-Biblia.
Mahubiri ya kufafanua humfanya mhubiri kuwa wa ki-Biblia kwani mhubiri huhubiri
kile kilicho katika maandiko ya eneo husika. Mhubiri huwa anajikita katika
mkutadha wa aya, sura na kitabu chote kwa ujumla. Hivyo kiini cha kitabu ndicho
ambacho hubeba mahubiri yake yote.
Mambo ya kuzingatia katika kutayarisha
mahubiri ya kufafanua.
I. Kwa umakini cuagua kifungu cha maandiko
kinachostahili. Hakikishwa kwamba kifungu hicho
kitahudumia uzima na uwezo wa wasikilizajiwao.
1.
Usichague somo kwa sababu linakuvutia au kukupendeza.
2.
Usichage somo ambalo litazaa machafuko, mgawanyiko na mashindano.
3.
JItahidi kufanyika njia ili Mungu akupitie ili Mungu akupitie ili aweze
kuongea Neno lake
kwa watu wake kwa kupitia
wewe.
4.
HIvyo basi unawajibika kutafuta
kujua mawazo ya Mungu kuhusu watu wake ambao amekupa wajibu juu yao.
5.
Huduma hii ni moja ya heshima kuu uliopewa lakini pia ni wajibu mkuu
unaoogopesha sana.
Hivyo basi unapaswa kuifanya kwa umakini wa hali ya juu.
II.Tafuta ujumbe unaolingana na hali ya
watu ya wakati ule.
1.
Mungu kila mara huwa na ukweli wa
sasa ambao hutaka kunena na watu wake.
2.
Mungu hukusudia jambo maalum kwa kila kundi la waamini
3.
Jifunze kujua kile Mungu anacho kwaaji ya kusanyiko kwa kilac wakati.
III. Jifunze sura ya kitabu kwa umakini.
1.
Soma sura unayo shughulikia mara nyingi mpaka umeielewa vizuri.
2.
Soma kwa uangalifu mstari hadi mstari.
3.
Kila kunapokuwepo na uhusiano wa wazi kati ya kifungu hicho na kifungu
kingine unapaswa kusoma kifungu hicho ili uweze kupata maana zaidi. Maandiko
hufasiri maandiko.
4.
Jenga usikivu kwa sauti ya Roho mtakatifu ili kupokea ufunuo toka kwake.
Tunia
vitabu vya rejea ili kupatamsaada zaidi. Mfano. Itifaki ya Biblia, Kamusi ya
Biblia, Biblia ya Tafsiri nyingine.Nk
IV. Kusanya taarifa muhimu.
Waweza kupata
vitu vingine muhimu vya kuhusisha kwenye somo lako kwa kutumia mbinu ya
maswali na majibu kama
ifuatavyo.
1.
Nimewahi kusikia au kusoma nini juu ya somo hili?
2.
Roho mtakatifu amewahi kunionesha nini juu ya somo hili?
3.
Nimewahi kuona nini chenye uhusiano na somo hili ?
4.
Nimewahi kuwa na mawazo gani juu ya somo hili ?
Naweza kupata
habari zaidi ju ya somo hili kwa nani au
wapi ? kueleweka.
5.
V. Tambua kiini cha somo lako.
1.
Daima tafuta kugundua kiini cha sura unayoshughulikia.
2.
Tafuta kujua kile Roho mtakatifu alikusudia kuwasilisha alipoivuvia sura
hiyo.
3.
Gundua undani wa somo hilo.
4.
Baini kile Mungu anataka kusema na watu wake kupitia sura hiyo.
VI.Kuwa na Lengo kamili.
Lengo
lako daima lapaswa kuendana kikamilifu
na lengo la Mungu.
1.
Hakikisha kwamba Umegundua kile Mungu anataka kutoa kupitia maadiko hayo
na kisha jizamishe katika kile Mungu anataka kufanya.
2.
Unapaswa kuhisi kile Mungu anachohisi Mungu humshirikisha mhubiri moyo
wake na akili yake ili waweze kufanya kazi pamoja. Unapaswa kuchangamka.
3.
Fanyika chombo cha Mungu cha kupitishia ujumbe wake kwenda kwa watu
wake.
4.
Kumbuka hukuitwa kushiriki mawazo yako na watu bali kuwashirikisha watu
mawazo ya Mungu.
VII. Zungumza kulingana na ujuzi wako
mwenyewe.
1.
Usitoe nadharia toa uhai. Hubiri kile ulicho na uzoefu nacho.kile
ambacho umekifanyia kazi . wapaswa kuwa mtu kwa kwanza kula matunda ya kazi
yako.
2.
Umeitwa kuwa barua Sio tu kwamba unataikwa kuuhubiri ukweli bali pia
unatakiwa kuufanyia mazoezi na kuuonesha kwa matendo.
3.
Unapaswa kuwa mfano hai wa yote unayoyahubiri.
VIII. Upe maana ujumbe wako.
1.
Unawajibika kwa uwezo wako wote, kuhakikisha kwamba maana ya kweli na umuhimu wa maandiko unakuwa
wazi. Na wakueleweka kwa wasikilizaji.
2.
Daima jitahidi kuufanya ujumbe wako kuwa rahisi.
3.
Hivi ndivyo Yesu alivyofanya Hii
ilisababisha huduma yake kuwa na nguvu na mafanikio.
4.
Alichukua mambo yaliyokuwa mafumbo na
na akayaweka rahisi sana.
5.
Wahubiri wengine huyachukua masomo rahisi sana
na kuyafanya mafumbo magumu sana kiasi cha
kutoeleweka kwa wasikilizaji wake au kuelewa kidogo.
IX.Fanya ujumbe wenye kutekelezeka.
1.
Daima unapohubiri jitahidi kuonesha wazi
wasikilizaji wako jinsi wanavyoweza kuutendea kazi ujumbe wako.
2.
Jitahidi kutoa ushauri wa kimatendo kuhusu watu wanavyotakiwa kumwitikia
Mungu kwa namna ya kufaa.
3.
Husianisha mahubiri yako na maazimio yako kimatendo ambayo yaweza
kuwafanya watu kuwa watendaji wa Neno na si wasikilizaji tu.
Zoezi
1.Eleza maana ya
mahubiri ya kufafanua.
2. Tathmini
ubora na udhaifu wa mahubiri ya kufafanua.
3. Taja mambo
mengine muhimu ya kuzingatia katika mahubiri ya kufafanua.
4. Chagua sura
mojawapo ya injili ya Yohana na kisha andaa mahubiri ya kufafanua kutokana na
sura hiyo na kisha hubiri kwa dakika kumi.
III.
MAHUBIRI JUU YA MAISHA YA WATU.
A.Utangulizi
Hii huhusu hadithi ya maisha ya watu. Kwa hiyo
njia hii huhusisha mafunzo juu ya maisha ya watu mbalimbali tunaosoma habari
zao katika Biblia. Kila hadithi ya mtu iliyoandikwa katika Biblia ina umuhimu
kwetu. Maisha ya kila mhusika aliye kwenye Biblia yana mafunzo kadhaa ambayo twaweza kujifunza. Kila habari iliyoandikwa kwenye Biblia ipo
kutufundisha kitu fulani ambacho ni cha thamani sana. 1Kor
10:1-11.
Mhubiri huchagua
mhusika mmojawapo wa wahusika walio katika Biblia na kujifunza kwa kina kila
kitu kilichotoke katika masiha ya mhusika huyo, tangu kuzaliwa kwake mpaka kufa
kwake. Pia mhubiri hutakiwa kujifunza kuhusu nasaba na mbari ya mhusika huyo
ili aweze kufahamu vizuri vitu vilivyomjenga na kumkuza mhusika, kisha
hutayarisha mahubiri juu ya mhusika huyo na kuhubrikatika kusanyiko lake.
Mafundisho ya
wahusika wa Biblia ni ya kushangaza na ya kuvutia.
Katkia aina hii
ya mahubiri, mhubiri hupaswa kuchaqgua mhusika mmoja na kusoma habari zake zote
zilizo kwenye Biblia na kisha huandikia kila wazo analolipata. Hapa mhubiri
anapaswa kusoma kumbukumbuzote za mhusika katika Biblia.
Baada ya kusoma
kumbukumbumbu hizo unapaswa kuanza kuweka pamoja mawazo yote unayoyapata katika
utaratibu wa miaka yaani jinsi matukio yalivyotokea ya mhusika huyo.
B. Faida za
mahubiri juu ya maisha ya watu.
I.Hufunua ukweli
wa maisha. Biblia imeelze wazi maisha ya wahusika kama
yalivyokuwa pale kuficha chochote. Imeeleza mafanikio yao
na madhaifu yao.
Ukweli wa maisha ya wahusika umewekwa wazi
na kwa uhalisia.
Wengi wa
mashujaa wa biblia wanahitilafu zao za kibinadamu.Twajua kuwa walikuwa wanadamu
kama sisi na walikutana na majaribu kama sisi.
Katika visa
vyote vya historia kuna mtu mmoja mkamirifu ambae ni Yesu kristo pekee. Hata
mashujaa wakubwa wa imani walikuwa na hitilafu zao. Hii inatupa kujua kwamba
wao si tofauti na sisi.
Ni mifano ya
kujifunzia. Ni mifano na msada kwetu.
Tunaweza kujifunza kutokananayo kuliko ujuzi wetu wa uchungu.
C. Mambo ya
kuzingatia
a)
Jifunze kuzaliwa kwa huyo mtu.
b)
Tafakali hali na mazingira aliyolelewa.
c)
Angalia uhusiano wake na Mungu katika maisha yake.
d)
Angalia jinsi alivyo wajibika kuhusu uhusiano wake na Mungu.
e)
Baini vitu alivyojifunza kutokana na mahusiano yake na Mungu.
f)
Tathimini mafanikio yake. Jifunze vitu vilivyomfanya afanikiwe.
g)
Tazama maeneo aliyokosea kama yapo. Na
jifunze vitu vilivyomfanya akosee.
h)
Toa hitimisho kile tunachoweza kujifunza kutokana na maisha ya mtu huyo.
Mambo hayo yote
yanavutia na ni yenye vitu vingi vya Kutufundisha ambayo twaweza kujifunza kutokana na watu hao. Tunaosoma habari za
maisha yao
katika Biblia.
D. Hatua za kufuata katika kuandaa mahubiri juu ya
maisha ya watu.
I. Chagua mtu au msusika toka kwenye
Biblia. Unapaswa kuanza na watu mashuhuli katika biblia ambao habari zao
ziko wazi kabisa.kama vile Ibrahimu,Musa,Samweli, Daudi, Yusufu, Debora, Miriamu, Mariamu,
Dorkasi, Paulo, Petro. N.k.
Hawa ni baadhi
ya watu ambao matendo yao
yameyanyika kuwa nuru katika historia ya dushusiano kati ya Mungu na mwanadamu.
Kuna mambo mengi
sana ambayo twaweza kujifunza kutokana na maisha
yao. Aina hii
ya mahubiri ni nzuri sana, kujifunza toka kwa
wacha Mungu wenzetu waliotutangulia katiki wito na huduma hii ni jambo la
msingi sana.
1Kor 10.1-11.
II. Chunguza maisha yake.
Anza kwa kusoma
hadithi inayoelezea kuzaliwa kwa mtu huyo. Tafuta maana ya jina lake. Kwani
jina lina maana sana
ki-Biblia. Angslia kwa umakini kusudi la Mungu katka maisha yake. Ili uweze kuvumbua vitu vingi unapaswa kujiulza mawsali fafuatayo:
1.
Mungu alitaka kutekeleza nini kupitia mtu huyu ?
2.
Je Mungu alifanya nini ili kusudi lake lijulikane
kwa mtu huyu?
3.
Mtu huyu aliitikia vipi Mungu alipomjulisha kusudi lake?
4.
Tunaweza kujifunza nini kutokana na Mungu kuhusika katika maisha yake ?
5.
Kuna tahadhari zozote ambazo tunapaswa kuzichukua ?
6.
Je siri ya mafanikio yake ilikuwa nini ?
7.
Je mwisho wa maisha yake ulikuwaje ?
III. Chambua somo na kisha hubiri.
Baada ya
kujiuliza maswali hayo na kupata majibu
utakuwa umepata vitu vingi ambavyo waweza kuvichambua kwa umakini na kuandaa
somo kisha na kulihubiri somo hilo
katika mpanglio na mtiririko Mzuri wwa mawazo.
Mwombe Roho
mtakatifu akupe ufunuo zaidi unapokuwaukihubiri somo lako na lifanye somo lako
kuwa na uhalisia katika maisha ya sasa ya wasikilizaji.
Zoezi
1.Eleza maana ya
mahubiri ya wahusika au maisha ya watu.
2. Tengeneza
orodha ya watu mashuhuri walio katika
Biblia. Orodha hiyo ihusishe wanawake na wanaume.
3. Tathmini
ubora na udhaifu wa mahubiri ya wahusika.
4. Chagua
mhusika mmoja wa kike au wa kiume na kisha andaa mahubiri kwa kumtumia mhusika
huyo na kisha hubiri kwa dakika kumi.
IV.
MAHUBIRI YA MIFANO HALISI NA VIVULI.
Huu ni ujuzi
unaohusu kuweka wazi au kuchimbua na kuwasilisha kweli uliojificha wa mifano mbalimbali katika Biblia.
Mfano ni kitu,
mtu au tukio ambalo kinabii ni ishara ya kitu au mtu fulani.atakaetokea baadae.
Inafanana au ni mfano wa Yule mtu au tukio.
Katika matumizi
ya biblia ina maana ya mtu wa bibliaau tukio litakaloonesha kitu fulani
kitakachotokea.
Mfsno
mwanakondoo katika kitabu cha Kutoka ni mfano wa Bwana Yesu.Kila kitu kuhusu kondoo wa pasaka
kiunabii kilkuwa na maana ya ukombozi ya wajibu ambao Bwana yesu Kristo
angetimiza.Yn 1:29.
Mifano ya biblia
mara nyingi inaonekana kama kivuli(type) cha
mambo yanayokuja baadae.
Ebr 8:5,10:1.
Siku takatifu
pia katika agano la kale zilikuwa vivuli ju ya mambo ambayo yalikuwa yanakuja.
Kol 2:17. Hizo
siku takatifu hazikukamilika zenyewe sehemu ya kusudi la kutimizwa kwake ilikuwa ni kutanguliza sura ya kinabii ya
vitu ambavyo vilikuwa bado vinakuja.
Kanuni za kutumia.
a. Unapojaribu
kwa mara ya kwanza kufundisha kwa
kutumia mifano ya kwenye Biblia, zingatia misingi ifuatayo.
I. Tumia mifano rahisi zaidi. Anza na
mifano rahisi mabayo maana yake iko wazi.
II.Endelea na tafsiri ya wazi. Usijaribu kutafsiri kila kitu.Elezea
ukweli wote kama ulivyo na wala si kutafuta
kila kipengele chake na kukielezea kwa undani.
III. Usitumie maneno makavu. Usitumie
mifano ya kufundishia kama kanuni.
IV.Sisitiza ukweli wa msingi..Usitumie
nafai uliyonayo kwa kutoa mifano ya kufundishia. Mifano itumike kusisitiza
mafundisho na si kutumia kama chanzo cha
ukweli.
V. Uwe tayari kusahihishwa. Uwe tayari
kusahihishwa na kukosolewa na wale waliokomaa kuliko wewe ili uweze kujifunza
zaidi.
4. Kuelezea kusudi.
Ni njia ambayo
kwayo mhubiri hupanua maana ya ukweli ulio
katika kifungu maalum cha maandiko.
Unatafuta naman ya kuuweka wazi ukweli ambao umejificha ndani ya kifungu. Hii
njia nzuri sana
ya kufundishia kusudi lote la ki-Mungu. Mdo 20:27.
Hapa mhubiri
aweza kuchukua kitabu cha Biblia na kuelezea
maana yake sura baada ya sura.
Zoezi
1. Eleza maana
ya vivuli na mifano.(Types).
2. Taja hatua za
kufuata katika kutayarisha na kuhubiri mahubiri ya mifano na vivuli.s
3. Tathtmini
ubora na udhaifu wa mahubiri ya mifano na vivuli.
4. Tayarisha
mahubiri ya mifano na vivli na kisha hubiri kwa dakika kumi mbele ya wanafunzi
wenzako.
V.
MAHUBIRI YA MADA.
Aina hii ya
mahubiri hukusudiakutoa kiini maalum kwa
hadhira.Mhubiri huchagua somo fulani kisha huchunguza kila kitu ambacho Biblia
inasema juu ya somo hilo.
Baada ya kuchunguza na kuchambua kweli hizo huandikwa katika mapngilo wa
somo.Mhubiri hupitia vifungu mbalimbali vya maandiko vinavyohusu somo hilo.
Aina hii ya
amhubiri huhitaji maandalizi ya muda mrefu na utulivu mwingi. Pia huwasilishwa
katika mfululizo wa vipindi kadhaa na si kimoja, kwa sababu ni vigumu kupitia
kweli zote zilizo katika somo kwa kipindi kimoja tu.
Mfano wa mada za kuhubiri.
1. Upendo wa
ki-Mungu
2. Ubatizo wa Roho
mtakatifu
3. Maombi ya
kufunga.
4. Nguvu ya usaidizi.
5. Vita vya kiroho.
6. Kutambua
Ulimwengu wa roho.
7. Kutembea katika
mamlaka.
8. Nguvu ya
madhabahu.
9. Kushughulikia
majira na nyakati.
10. Kutii mamlaka.
Mambo ya kuzingatia katika mahubiri ya
mada.
1.
Uwe na ufahamu kwa kutosha juu ya somo husika.
2.
Fanya maandalizi ya mudamrefu nay a kina
3.
Unapaswa kuwa na lengo mahususi la mahubiri yako.
4.
Gawa somo katika vipengele vidogovidogo.
5.
Kila kipengele laima kiwe na maandiko yanayokithibitisha na kukielezea
6.
Andiko liendane na dondoo
unayoitoa.
Zoezi.
Somo hili
lipo kimatendo zaidi. Kila mwanafunzi ashiriki katika kufanya mazoezi ya
kuandaa mahubiri na ahubiri katika dakika zilizopendekezwa au mwalimu
atakazopanga kulingana na muda uliop.
Mwalimu anatakiwa kusimamia na kusahihisha
kazi za wanafunzi na kutoa marekebisho katika maeneo ambayo wanafunzi
hawajafanya vizuri.
1.Andaa Ujumbe
kwa kutumia aina ya mahubi ya mada na
kisha hubiri mkuano kwa dakikika arabaini. Chagua mada yoyote.
2.Taja ubora na
udhaifu wa mahubiri ya mada.
3. Taja mambo
mengine matano muhumu ya kuzingati
katika kuandaa mahubiri ya mada.
4. Toa tofauti
iliyopo kati ya mahubiri ya mada na
mahubiri ya kufafanua.s
VI.MAHUBIRI
YA MATUKIO.
Mahubiri ya
matukio ni kipengele katika mahubiri ya maada, lakini kutokana na umhuhimu wake
tumekitenga na kukielezea peke yake.
Mahubiri
haya ni mahubiri ambayo huandaliwa
kutokana na tukio lilipoau ambalo litafanyika katika kipndi fulani.
Kiini cha
mahubiri haya huwa ni tukio ambalo linafanyika katika ibada hiyo.Mfano wa
matukio hayo ni
Tukio la,
1.
Kusimikwa kwa uongozi wa kanisa.
2.
Ndoa au kumuaga bibi arusi.
3.
Kubariki watoto.
4.
Ushirika mtakatifu
5.
Kuweka wakfu vitu mbalimbali.
6.
Kuhitimu mafunzo.(graduation)
7.
Msiba na mazishi.
8.
Sikukuu mfano Pasaka, mwaka mpya, N.k
Mambo ya kuzingatia
1. Mahubiri haya
yanapaswa kuendana na tukio husika.
2. Mhubiri anatakiwa
kufahamu ratiba nzima ya tukio hilo
au shughuli hiyo.
3. Mhubiri ahubiri
kulingana na tukio husika.
4. Mhubiri aepuke
kutumia muda mwingi katika mahubiri.
5. Mhubiri ahubiri
kwa lugha itakayoeleweka na kusanyiko lote na lugha yapaswa kuwa rahisi.
6. Mahubiri yapaswa
kugusa kusanyiko lote.
7. Mhubiri anapaswa
kubiri kwa upendo.
8. Mhubiri azingatie
ratiba ya tukio.
ZOEZI.
1. Chagua tukio mojawapo na kisha
andaa mahubiri juu ya tukio hilo na hubiri kwa dakika 10
.2. Taja mabo mengine kumi ya kuzingatia
katika mahubiri ya matukio.
3.Eleza ubora na udhaifu wa mahubiri ya matukio.
1. MAHITAJI YA MUHUBIRI:
a. Anapaswa kuwa
ameokoka yaani amezaliwa mara ya pili.
a. anapaswa kuwa
na wito kamili na uliowazi kwajijli ya
kazi hii na sii taaluma tu.
Anapaswa kuwa
amejazwa Roho mtakatifu.
Anapaswakuwa na
wito uliowazi kwake na kwa watu wengine pia.
3. Mhubiri anapaswa kuboresha utu na wito
wake kwa njia zifuatazo:
I.kuwa na
ushirika wa karibu na Mungu daima.
a)
Maombi na kutafakari Zab 1, Yosh 1:8.
b)
Kuishi maisha matakatifu.
c)
Kuwa mnyenyekevu daima.
II Anatakiwa kujifunza daima.
Neno la
Mungu na vitabu vinginevyo vizuri.
a)
Panga muda wa kusoma (soma kwa bidii).
b)
Pata chakula kwajili yak o mwenyewe.
c)
Pata chakula kwaajili ya watu wengine.
d)
Hudhuria makongamano na semina mbalimbali.
e)
Jifunze toka kwa wahubiri wengine wakubwa na wazuri waliokutangulia.
III.Jifunze kutokana na watu wanaokuzunguka
na mazingira yao.
a)
Tazama na soma watu wanavyoishi, matatizo wanayokutana nayo.
b)
Fungua macho yako kujifunza kila mahali.
IV.. Endeleza vipawa vyako vya asili.
Kil;a
mtu anacho kipaji cha asili. Ni muhimu kuendeleza kipaji ulichonacho kwaajili
ya utukufu wa Mungu. Mfano wa viapji vya asili ni Kuimba, kupiga muziki,
kushauri, n.k. Vipaji vyote vyaweza kuendelezwa kwa njia ya mafuzo na mazoezi.
Hivyo hakikisha unakuza na kuendeleza kipaji chako cha asili.
V..Tunza afya yako. Ni muhimu kwa
muhubiri kutunza afya yake kwanibila kuwa na afya bora muhubiri hataweza
kutimiza wito wake kwa ufanisi. Pai ni
jambo jema kwa muhubiri kufuata ushauri wa kitaalamu yaani kuchunguza afya yake
mara kwa mara ili kushugulikia mapema kama kuna dosari zozote za kiafya kiwa
bado change. Pia ili muhubiri aweze kuwa na afya bora anatakiwa kufanya
yafuatayo:
i.
kula chakula bora.
ii.
Kufanya mazoezi mra kwa mara. Mfano
kukimbia, kuruka, kutembea, N.k
iii.
Kuwa na muda wa kupumzika.( Muhubiri ni lazima awe na muda wa kutulia na familia yake. Pia mhubiri
anapaswa kuwa na likizo.)
VI. Vipaumbele vya muhubiri. Unapaswa
kutambua vipaumbele na uviheshimu ili uweze kuwa na ufanisi katika huduma na
wito wako. Vpaumbele hivyo ni:
a)
Mungu.
b)
familia.
c)
Huduma
d)
Watu wengine.
Kila
kipaumbele kipe nafasi yake. Usipofanya hivyo utumishi wako utatyumba.
VII. Ni lazima amtegemee kikamilifu Roho
mtakatifu.
“ Atatwa katika yaliyo yangu na kuwapa ninyi.
Yn 14:26, 16:13-14.
Hivyo ni lazima mhubiri ajifunze kumtegemea
Mungu kiamilifu;
a)
Katika maisha yake ya kila siku.
b)
Katika masomo yake.
c)
. Katika maandalizi na matayarisho.
-
Katika kuandaa hotuba za kuhubiri.
-
Katika kuandaa matirio ya kutumia katika kuandaa hotuba zake.
-
Katika kuwasilisha hotuba zake.
a)
Kwa kutumia stadi na ujuzi pekee wa homiletics na akili yako pekee
kusanyiko lako litabaki tupu na ukiwa.
b)
Ni Roho mtakatifu pekee anaewweza kumtia nguvu mhubiri kuufikia ushindi
wa kiroho Mdo 1:8.
c)
Ni Roho mtakatifu pekee anaeweza kubadilisha na kuhuisha wasikilizaji
wako. Yn 16:7-8.
d) Mhibiri unapaswa daima kumtegemea
kikamilifu Roho mtakatifu katika kazi na wito wako wa uhubiri. Hakikisha
unashirikiana nae kikamilifu iliuweze kuwa na ufanisi katika wito na huiduma
yako.
*Roho
mtakatifu aweza kuwa msaada kwa mhubiri
lakini yeye ni kama hua….
MADA YA PILI.
A. mhubiri ni
mtangaza ujumbe wa Mungu.
-Yeye ni msemaji
wa Mungu. Husimama katika nafasi ya mungu na kuzungumza kwa niaba yake Mungu.
B. Biblia ndiyo
asili ya ujumbe. Ujumbe wowote uaouhubiri nilazima utokane na Biblia nje ya
Biblia si mahubiri bali ni masimulizi tu.
-Ikiwa kuhubiri
ni kutangaza ujumbe wa Mungu mhubiri anapaswa kwenda mahali Mungu
alipoongea mara nyingi na waziwazi yaani
“Biblia”
Kwa njia nyingine kuhubiri ni kuipa Biblia
sauti.ni kuacha Mungu aongee mwenye koa kwa Neno lake.
Kwa nini Biblia
peke yake? Kwanini si kitu kingine toka
vitabu vizuri vya kikristoau toka magazeti au maelezo na masimulizi ya mtu
maarufu na aliye mkuu.
1. Biblia ni
maoni ya Mungu kwa kila jambololotelililotolewa.
(Mhubiri aliye
kuwa amekosolewa kwaajili ya hotuba yake alisema “hata mimi sikuipenda pia
lakini haikuwa maneno yangu na nilikuwa
sitoi mawazo yangu bali kile Mungu amesema katika Neno lake. Kwahiyo nilitoa
mawazo ya Mungu na si yangu.).
Kuhubiri hotuba
ya ki-Biblia humpa mhubiri ujasiri mkubwa. Kutangaza kwa nguvu;
·
Biblia inasema ………………….
·
Mungu anasema…………………
2. Neno la Mungu
lina nguvu. Wab 4:12.
3.Neno la Mungu
ni kama mbegu.sBiblia hukutana na kila hitajila mwanadamuna matatizo yake yote
yanayomkabili.
5. Inampendeza
Mungu- Neno lake lililovuviwa amri yake
ilikuwa wazi
“Enendeni
mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi na muwafundishe kuyashika yote
niliyowaamuru”
6. Roho
mtakatifu hulithibitisha Neno la Mungu.
C. jinsi ya
kupata maandiko ya Kuhubiri.
Mwombe Mungu
Akupe ujumbe waq kuhubiri.kissha pokea andiko toka kwa Mungu kuhusu mahubiri
hayo kwanini yeye Mungu anajua mahitaji ya watuya sasa yanayotakiwa
kushughulikiwa……………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
D. Namna ya
kutumia maandiko kwa usahihi.
Kufasili na
kutumia maandiko matakatifu kwa maana
yake halisi ni kazi moja muhimu na takatifuambayo mhubiri anawajibu wa
kuifanya.
1. Usipindishe wala kugeuza maana ya andiko
ili kulifanya andiko likubaliane na mawazo yako.
2.Usichukue
sehemu ya andiko na kuifanya iseme kitu ambacho hakiendani na mkutadha wake
ambao ambacho mkuadha hauoneshi kuwa ni maana yake halisi.
3. Soma andiko kwa umakni (zingatia
sarufi na misemo iliyomo katika andiko) na ulitafakari katika maana yake
halisi.
- Baini aina ya tungo zilizotumika na
aina za maneno yaliyotumika kuunda tungo hiyo.
-Tazama maneno
maalumu(Key word)yanayotokeza katika andiko unalotafakari.Mfano DAmu, Msalaba, Yerusalemu N.k.
-Kuwa makini kutazama tamathali za semi
zilizotumika au kujitokeza. Mfano. Misemo, nahau, tashibiha, tashihisi
tashititi, tafsida ,methali n.k.
4. Soma andiko katika mkutadha wake wa
sasa. hapa unatazama mkutadha wa
msitari, aya na sura ya andiko.
5.Soma andiko katika mkutadha wake wote.
Hapa unatazama mkutaqdha wa kitabu. Waweza kutumia mAswali kadha katika
kutazama mkutadha wake mfano Ninin
dhamira ya kitabu au waraka huu wote? Tazama historia, jografia na utamaduni wa
wakati wa Biblia hii daima yaweza kuwa msaada.
* Daima kumbuka kuwa mafundisho ya Biblia
yanapatana na hayapingani kamwe. Hayajipingi yenyewe kwa yenyewe lakini ufuno
wake ni endelevu.
*Mafundisho ya agano la kale ni lazima
yafasiliwe katika nuru ya Agano jipya. Kushindwa kufanya hivyo kumesababisha
kuzaliwa kwa mafundisho mengi ya uongo.(Religious cults).
Mfano. Kutunza sabato, kutokula baadhi ya
wanyama, Kuabudu sanamu, kuoa mitala N.k
D. mawazo mawili
potofu kuhusu mahubiri.
Kuna dhana mbili
potofu ambazo zinajitokeza katika uwanja na taaluma ya mahubiri mawazo hayo ni:
a. Maaandalizi si lazima. Wazo la
kwanzalenye makosa ni kwamba maandalizi
si lazima na huonesha kukosa imani kwa mhubiri. Watu wenye kushikilia msimamo
huu hufikili kwamba imani ya kweli
hutupilia mbali jitihada yoyote
inayojaribu kuandaa akili na hiyvo husimama mimbarini wakiamini kwamba Mungu atawapa maneno ya
kusema.husimamia maawazo haya:
i. Roho mtakatifu atakupa unachohitaji
kuhubiri. Unapopanda mimbarini.
_- Zab 81:10 “ Fumbua sana kinywa chako name nitakijaza”(Hutumia
andiko hili kutetea msimamo wao.).
Pia husema
kwamba Yesu alisema kwamba “Msifikirifikiri nini cha kusema maana mtapewa
kinywa cha usemi saa ili ilie mnapotakiwa kusema”
Unapoyachunguza kwa umakini maandiko hayo
utagundua kwamba maandiko hayo
wanayafasili nje na mkutadha wake na na kulazimioshwa yaseme kile ambacho
hayamaanishi.
*Mahubiri ni
kamana jengola kiroho ambalo linatakiwa kusanifiwa na kuandaliwa chini ya
uongozi wa Roho Mtakatifu. Roho
mtakatifu ndiye mhandisi mkuu wa mahubiri.
b. Uwezo wa mtu unatosha. Kuweka mkazo
katika matayarisho na kutegemea uwezo
wa kibidanu tu. Wahubri wanaoshikilia
msimamo huu hudai kwamba maandalizi peke
yake yanatosha na huweka mkazo
kwenye matayarisho pekee.Kumtegemea Roho
mtakatifu huwa ni kudogo sana au hakuna kabisa, bali tumaini la mtu binafsi
ambalo ni matokeo ya kujifunza na kuendeleza uwezo wa asili.
Ujumbe wa namna
hii waweza kuwa mzuri kabisa lakini hauwezi kuleta matokeo yatakikanayo daima.
Kwani ni Roho mtakatifu pekee ndiye anaeweza kuleta badiliko katika maisha ya
waikilizaji wako. Bila yeye mahubiri huwa ni maiti na haiwezi kuleta uhai kwa
sababu ni uhai wenye uwezo wa kuzaa uhai.
*Roho mtakatifu
huuhuishaujumbe na kuletaq matokeo yaliyokusudiwa na Mbingu katika maisha ya
wasikilizaji.
Ili mhubiri
aweze kuhubiri sawasawa anapaswa kuwa na maansdalizi ya kutosha katika kuuandaa
ujumbe wake kwa kusoma, kutafakari na kuchambua kweli zote zilizomo katika
ujumbe wake. Lakini hayo yotec anapaswa kuyafanya akiwa katika hali ya maombi.
Mhubiri anapaswa
kumsikiliza Roho mtakatifu klwa kina na kupata uongozi kwake na kutaka Roho
mtakatifu amshirikishe kile anachotaka kusema na watu wake na kukifanyia
uchambuziyakinifu katika hali ya maombi ili aweze kukiwasilisha kwa ufanisi.
·
Mhubiri anapaswa kutambua kwamba yeye hana watu wala si Chanzo cha
ujumbe. Kwasababu hiyo anatakiwa kumsikiliza mwenye watu na aliye chanzo cha huo ujumbe na kusimama
katikati kwa uaminifu kuwafikishia watu kwa usahihi kile mwenye watu anachotaka
kiwafikie watu wake.
·
Mhuibiri anapaswa kutambua kwamba
kazi ya kuhubiri ni takatifusana na ni kazi nyeti ambayo yapaswa kufanywa kwa
umakini, uaminifu na unyeyekevu mkuu.
·
Mhubiri mwenye kutegemea juhudi zake na uwezo wake wa asili atakuwa ni
muhubiri kilema na halikadharika mhibiri mweye kutegemea kupewa ujumbe akiwa
mimbarini atakuwa ni kilema.
·
Vyote viwili vyapaswa kwenda pamoja, maombi na matayarisho.Kwa
sababu mahubiri ni matokeo ya mawasiliano na ushirika mzuri kati ya Roho mtakatifu na mhubiri.
Aina za mahubiri.
Katika kipenele hiki tutaeleza aina saba za
mahubiri. Ni vizuri kwa mhubiri kufahamu aina zote za mahubiri. Hii itamsaidia
kuwa na uhuru waq kutumia ainayoyote
katika huduma yake na kufanya huduma yake kuwa ya kuvutia kwa watu
wanaomsikiliza.
2. Mahubiri ya mada.
Aina hii ya
mahubiri hukusudiakutoa kiini maalum kwa
hadhira.Mhubiri huchagua somo fulani kisha huchunguza kila kitu ambacho Biblia
inasema juu ya somo hilo.
Baada ya kuchunguza na kuchambua kweli hizo huandikwa katika mapngilo wa
somo.Mhubiri hupitia vifungu mbalimbali vya maandiko vinavyohusu somo hilo.
Aina hii ya
amhubiri huhitaji maandalizi ya muda mrefu na utulivu mwingi. Pia huwasilishwa
katika mfululizo wa vipindi kadhaa na si kimoja, kwa sababu ni vigumu kupitia
kweli zote zilizo katika somo kwa kipindi kimoja tu.
Maoni